Mwanamke aliyekamatwa akiwa Uchi,Afikishwa Mahakamani kwa Tuhuma za Uchawi. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, August 10, 2013

Mwanamke aliyekamatwa akiwa Uchi,Afikishwa Mahakamani kwa Tuhuma za Uchawi.

       Kamanda Leonard Paulo-Geita.
JESHI la polisi mkoani Geita limemfikisha mahakamani Bi,Sophia Ngeleja (65) mkazi Butundwe wilayani Geita anayedaiwa kukamatwa akiwa uchi wa mnyama nyumbani kwa Bahabi Shomari (30) mkazi wa kijiji Mkuyuni wilayani Chato August 4 majira ya saa 03:00 usiku.

Mtuhumiwa  Sophia Ngeleja alisomewa shitaka lake katika mahakama ya wilaya ya Chato August 5 mwaka huu na mwendesha mashitaka wa polisi,mkaguzi msaidizi wa polisi,Mkwasi Rashidi mbele ya hakimu mkazi mfawiidhi wa mahakama ya Chato,Bw.Jovith Katto.


Mwendesha mashitaka alidai kuwa mtuhumiwa anadaiwa kutenda kosa la kujihusisha na vitendo vya kishirikina August 4,majira ya saa 03:00 usiku nyumbani kwa Bahabi Shomari,mkazi wa kijiji cha Mkuyuni wilayani Chato,ambaye pia ni mtumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Chato ambapo siku ya tukio alikutwa akiwa uchi wa mnyama kitendo ambacho ni kinyume na sheria ya uchawi no.18 kifungu cha 3 na 5 ya mwaka 2002 kama ilivyofanyiwa marekebisho.

Kwa mujibu wa mwendesha mashitaka alidai kuwa mtuhumiwa alipelekwa Hosptali ya wilaya ya Chato kufanyiwa uchunguzi wa afya yake,ambapo uchunguzi wa kitabibu ulithibitisha kuwa afya na akili za mwanamke huyo ni timamu.

Mtuhumiwa alikana kosa na kupelekwa gerezani Biharamlo,baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana,ampo kesi hiyo imehairishwa hadi August 19 itakapotajwa tena.

ALIVYOKAMATWA.

Siku ya tukio August 4,majira ya saa tisa usiku,Shomari Bahabi akiwa nyumbani kwake amelala alisikia kishindo cha mtu nje katika mlango wa nyumba yake wa mbele,baada ya hapo alichungulia nje na kumuona mtu akiwa nje huku akiwa uchi “nilikuwa naona kama naota ila niliamua kufungua mlango wa nyuma na kukimbia kwa mwenyekiti wangu wa kitongoji Bw.Kadri Mohamed ambaye pia ni jirani yangu nilikuja naye hadi pale kwangu na kumkuta Yule mama akiwa amenasa mlangoni,tuliwaamsha na watu wengine usiku huo” alieleza Bahabi

“baada ya kumhoji alidai alikuwa yeye ni mkazi wa Butundwe wilayani Geita  na alikuwa na  wenzake nane  ambao wamemuacha,alikuwa anaongea kwa ujasri pengine husingeamini,watu walizidi kuongezeka maana hapa kwangu ni njiani hata hivyo walikuwa wakipashana habari na kila mtu alitaka ashuhudie,tulikaa naye hadi saa 06:30 asubuhi polisi wa Chato walipokuja kumchukua,wakati wote huo alikuwa uchi”aliongeza.

Kwa upande wa mwenyekiti wa Kitongoji Bw.Kadri Mohamed alidai kwake ni tukio la kwanza na matukio hayo alikuwa akiyasikia mikoa mingine ila hakuwahi kuamini hadi lilipotokea kwenye kitongoji chake” siku hiyo saa tisa wakati Shomari ananiamsha sikuamini nilifikiri amechanganyikiwa hadi nilipofika kwenye tukio na kumkuta mtu akiwa uchi” anasema kwa kusikitika.

nilipofika nilimuuliza jina lake maana hapa kijijini alikuwa ni mgeni,ndipo aliposema kwamba yeye ni Sophia Ngeleja na ni mkazi wa Butundwe,na kwamba alikuwa na wenzake nanae wamemuacha hivyo anaomba msamaha,sikuwa na la kufanya zaidi ya kupiga simu polisi maana nilijua wananchi wanaweza kumdhuru,polisi walifika na gari ndogo na kuondoka naye akiwa hana nguo”aliongeza Mwenyekiti wa kitongoji.

Aidha mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini  alidai kuwa mama huyo hakupigwa kutokana na kwamba kila mmoja aliyefika pale kuingiwa na hofu.

yaani mimi mwenyewe nilikuwa natetemeka maana ulikuwa kama muujiza ama mazingaombwe” alidai shuhuda huyo.


Na:Denice Stephano-Geita.  
0767925018

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad