|
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza La Mapinduzi akiweka udongo
katika kaburi la Marehemu Fr. Evaris Mushi katika mazishi
yaliyofanyka leo katika makaburi ya Kitope wilaya ya Kaskazini B Unguja.
|
|
Waziri
wa mambo ya Ndani Mheshimiwa Dr. Emmanuel Nchimbi akiweka udongo
katika Kaburi lwa marehemu Fr. Evarist Mushi katika mazishi
ambayo yamefanyika leo huko Kitope wilaya ya Kaskazini B Unguja.
|
Padri
Mushi amezikwa Zanzibar badala ya
kusafirishwa kwenda kwao Moshi mkoani Kilimanjaro, ambapo Askofu Shao: anasema
kwamba “Padri Mushi ameishi Zanzibar tangu akiwa na miaka 18 hivyo ni mkazi wa
Zanzibar... Hakuna sababu ya kusafirishwa.
Mimi
ndiye niliyekuwa mlezi wake hivyo hakuna sababu ya kumpeleka kuzika kwa askofu
mwingine.”
Katika
Hatua Nyingine , baada ya kuuawa kwa kupigwa risasi Padri Evarist Mushi Mjini
Zanzibar, Kanisa la The Pool of Siloam lililoko katika Shehia ya Kianga, Wilaya
ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja, limechomwa moto na watu wasiojulikana na
kuharibu madhabahu yake.
Kuchomwa moto kwa sehemu ya kanisa hilo, kumetonesha kidonda cha kifo cha Padri Mushi ambaye aliuawa kwa kupigwa risasi kichwani, Jumapili asubuhi mjini Zanzibar.
Padri huyo amezikwa leo.
Mchungaji
Msaidizi wa Kanisa hilo, Penuel Elisha alisema tukio hilo ni la pili kwa kanisa
hilo kwani mwaka 2011 zaidi ya watu 80 wakiwa na mapanga, nyundo na magongo
walilivamia na kulivunja kabisa.
Alilishukuru Jeshi la Polisi kwa kuwahi kuwasaidia katika tukio la jana.
Licha ya kutotaka kuonyesha uhasama na msikiti uliopo eneo hilo, Penuel alisema siku moja kabla ya tukio hilo viongozi wa msikiti huo walihoji uhalali wa kujengwa kwa kanisa hilo.
Alipoulizwa kuhusu kuwapo kwa uhasama kati ya msikiti na kanisa hilo, Imamu wa msikiti huo, Hassan Migirimu alikanusha akisema kuwa mzozo huo ulikuwa kati ya kanisa na Sheha Assed Mvita ambaye amefariki dunia.







No comments:
Post a Comment