Askari wakiwa katika
gari lao wakivinjari
katikakati ya jiji.
|
Waandamanaji
hao walipigwa marufuku licha ya kuwa waliomba kibali cha kuandamana ili
wamuombe DPP atoe idhini ya dhamana kwa kiongozi huyo ambaye ni Katibu wa Shura
ya Maimamu na Jumuiya za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda na Wenzake.
Kikosi cha mbwa
hakikuwa nyuma
kuhakisha amani
inakuwepo.
|
Kaimu
Kamanda wa Polisi kanda Maalum ya Dar es Salaam, Bw.Ahmed Msangi, alisema pamoja
na kuwa jeshi lake halina askari wa kutosha kuwalinda waandamanaji hao lakini
pia taarifa zilionyesha kuwa kuna baadhi ya watu wamepanga kufanya vurugu
kupitia maandamano hayo.
Waandamanaji
hao walipanga kuanza maandamano yao mara tu baada ya kumaliza sala ya Ijumaa
katika misikiti mbalimbali ya jijini kuelekea zilipo ofisi hizo.
Taarifa
zinasema waandamanji hao wameongeza msukumo wa kudai dhamana ya Sheikh Ponda na
wenzake baada ya Elizabeth Michael Msanii wa filamu anayetuhumiwa kumuuwa
msanii mwenzake Steven Kanumba kupewa dhamana hivi karibuni.
Sheikh Ponda
na wenzake 45 walitiwa nguvuni mwishoni mwa mwaka jana na kesi yao itaendelea
kusikilizwa Februari 25 wakikabiliwa na mashitaka manne likiwemo la kuchochea
vurugu na uvamizi wa eneo la kampuni moja isivyo halali.
No comments:
Post a Comment