Azam FC ya Tanzania yailaza Al Nasir Juba ya Sudan Kusini mabao 3-1 na kuanza vyema mashindano ya Afrika katika Kombe la Shirikisho . - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, February 16, 2013

Azam FC ya Tanzania yailaza Al Nasir Juba ya Sudan Kusini mabao 3-1 na kuanza vyema mashindano ya Afrika katika Kombe la Shirikisho .


Wachezaji wa Azam FC

 wakimpongeza Babbi

kufunga bao la kwanza

Katika mchezo huo.

Timu ya Azam FC ya Tanzania  imeanza vyema  mashindano ya Afrika katika Kombe la Shirikisho  baada ya kuilaza Al Nasir Juba ya Sudan Kusini  mabao 3-1  katika mchezo wa leo Februari 16,2013  kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.





Mshambuliaji kutoka Ivory Coast, Kipre Herman Tchetche  aliisaidia timu yake ya Azam FC  kufunga  mabao mawili ndani ya dakika za mwisho na kuipa ushindi timu hiyo.




Kwa matokeo hayo, Azam FC sasa inahitaji sare tu katika mchezo wa marudiano wiki mbili zijazo nchini Sudan Kusini, au kufungwa si kwa zadi ya tofauti ya bao moja ili kusonga mbele kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.




Aidha Ligi ya Mabingwa Afrika inaanza   kwa hatua za awali, Tanzania Bara inayowakilishwa na Simba SC ikianza kazi Jumapili dhidi ya Recreativo de Libolo ya Angola, wakati wawakilishi wa Zanzibar wakianza na Kedus Giorgis ya Ethiopia leo, Uwanja wa Gombani, Pemba.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad