Yanga SC na raha tupu kwa mashabiki wake huku Mgambo Shooting na Toto African zikifanya kile kisichotegemewa na wengi baada ya kuzinyuka Azam na Simba katika mechi za Ligi Kuu ya Tanzania Bara. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, November 11, 2012

Yanga SC na raha tupu kwa mashabiki wake huku Mgambo Shooting na Toto African zikifanya kile kisichotegemewa na wengi baada ya kuzinyuka Azam na Simba katika mechi za Ligi Kuu ya Tanzania Bara.

Yanga SC
Wana jangwani Yanga SC wameendelea kuwapa raha mashabiki wao baada ya kufanikiwa kumaliza vema mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kileleni zaidi  kufuatia leo kushinda mabao 2-0 dhidi ya wenyeji Coastal Union  Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga katika mchezo wa Ligi kuu VPL.


Yanga imemaliza mzunguko wa kwanza ikiwa na pointi 29  ikifuatiwa na Azam FC katika nafasi ya pili yenye pointi 24 na Simba SC nafasi ya tatu kwa pointi zao 23.




Mabao ya  Yanga yamefungwa na mshambuliaji wake wa kimataifa wa Burundi, Didier Kavumbangu na bao la pili, mfungaji akiwa ni Mganda Hamisi Kiiza .



Simba SC
Aidha hapo jana katika Ligi hiyo ya Vodacoma,bao la Dakika ya 73 la mchezaji Musa Saidi Kimbu, liliwapa ushindi ‘Wapwa’ wa Yanga, Toto African  wa bao 1-0 dhidi ya Simba SC katika Mechi ya Ligi Kuu Vodacom VPL,  iliyochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na huko Tanga Mgambo JKT ikawachapa Azam FC bao 2-1 na matokeo hayo yamewabakisha Yanga kileleni na kuzidisha pengo la uongozi wao.



Simba walicheza Mechi yao bila Kipa wao Nambari Wani Juma Kaseja ambae amepumzika baada ya kuletewa kashikashi na Mashabiki wa Simba walipofungwa na Mtibwa Sugar bao 2-0 katika Mechi yao iliyopita huko Manungu mkoani  Morogoro.



Mtibwa Sugar
Nao Mabingwa wa Ligi Kuu mwaka 1999 na  2000, Mtibwa Sugar walilazimika kusawazisha kabla ya kuichapa African Lyon mabao 3-1.



Mshambuliaji Abdulghan Gulam aliifungia African Lyon bao la kuongoza katika dakika ya 22 akiunganisha kwa kichwa krosi ya Jackson Kanywa.


Mtibwa Sugar waliamka na kusawazisha bao hilo katika dakika ya 32 kupitia Shabani Nditi akimalizia pasi ya kinda Hassan Ramadhani, ambapo dakika tatu kabla ya mapumziko Ally Mohamed alifunga bao la pili kwa Mtibwa akimalizia pasi ya Hussein Javu.


Kama hiyo haitoshi, mshambuliaji Javu alifunga bao la tatu kwa Mtibwa akiunganisha vizuri krosi ya Ally Mohamed katika dakika ya 90. 



Tanzania Prisons
Mkoani Mbeya; Wenyeji Tanzania Prisons walilazimishwa sare ya 1-1 na JKT Ruvu.



Katika mechi hiyo mshambuliaji Misango Magae alifunga bao la kuongoza katika dakika ya 10  lakini Jimmy Shoji aliisawazishia JKT Ruvu kwa shuti kali lililochana nyavu katika dakika ya 87.


Jijini Arusha; Timu ya Ruvu Shooting ilipata ushindi wao kupitia Seif Rashid aliyefunga mabao mawili na Michael Pius moja, huku Amiry Omary na Edmund Kashamika wakifunga mabao mawili ya JKT Oljoro iliyolala kwa mabao 3-2 kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Arusha.



Kagera Sugar
Mkoani Kagera; Kwa upande wa Kagera Sugar wenyewe walilazimishwa sare ya 0-0 na Polisi Morogoro kwenye Uwanja wa Kaitaba.



RATIBA MECHI ZIJAZO:


Jumatano Novemba 14


Mgambo JKT v Tanzania Prisons [Mkwakwani, Tanga]


Jumapili Novemba 18


Ruvu Shooting v Tanzania Prison [Mabatini, Pwani]



RAUNDI YA PILI YA VPL 2012/2013.

Januari 26


African Lyon v Simba [National Stadium, Dar es Salaam]

Mtibwa Sugar v Polisi Morogoro [Manungu, Morogoro]

Coastal Union v Mgambo JKT [Mkwakwani, Tanga]

Ruvu Shootings v JKT Ruvu [Mabatini, Pwani]

Azam v Kagera Sugar [Azam Complex, Dar es Salaam]

JKT Oljoro v Toto Africans [Sheikh Amri Abeid, Arusha]


Januari 27


Yanga v Tanzania Prisons [National Stadium, Dar es Salaam]

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad