![]() |
Magari yaJeshi la polisi mkoani Kagera. |
Mtoto mwenye umri wa wiki tatu katika eneo la Nakatunga wilayani Ngara mkoani Kagera amekufa kutokana na kiachoelezwa kuwa ni kunyongwa na baba yake mzazi aliyetabuliwa kw a jina la Adam Ibrahim.
Mama mzazi wa mtoto huyo Bi Ombeni Paschal amesema tukio hilo limetokea mwishoni mwa wiki iliyopita katika eneo la Nakatunga mjini Ngara.
Bi Paschal amesema mtoto huyo alipiga kelele wakati akiwa amepakatwa na baba yake ambaye alimrejesha kwa mama yake akiwa anatoka povu mdomoni kabla ya kufariki .
Mganga mfawidhi wa hospitali ya Nyamiaga wilayani Ngara Dr Rafael Rwezaura amesema wamepeleka sampuli kwa mkemia mkuu wa serikali ili kubaini chanzo cha kifo hicho.
Jeshi la polisi wilayani Ngara limethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba linamtafuta mtuhumiwa ambaye ametoroka.
![]() |
Tembo wanazidi kuuwawa barani Afrika kutokana na kuongezeka kwa biashara ya pembe nchini China |







No comments:
Post a Comment