Je Halmashauri ya wilaya ya Ngara mnaufikiriaje uwanja huu wa Kokoto?? - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, March 29, 2018

Je Halmashauri ya wilaya ya Ngara mnaufikiriaje uwanja huu wa Kokoto??

Muonekano wa eneo la kuchezea uwanja wa Kokoto ambao unatajwa kuwa ni Uwanja wa wilaya ya Ngara mkoani Kagera.

Licha ya kuidhinishwa kutumika kwa mashindano mbalimbali ya mchezo wa soka wilayani Ngara mkoani Kagera, Uwanja huu unaotajwa ni wa Kiwilaya uliopo Mjini Ngara, maarufu KOKOTO haukikidhi vigezo vya usalama kwa wachezaji na hata walau masharti 89 yaliyoanishwa na Fifa kuhusu usalama wa viwanja (89 Fifa Football Stadium Technical Recommendations and Requirements).
Eneo la Kuchezea katika Uwanja huo wa Kokoto.

Ikumbukwe kuwa , Viwanja vya soka ni mahali pa hisia za kimichezo na mvuto kwa watu wengi. Ni sehemu ambayo hutumiwa na maelfu ya watu bila kujali tofauti za itikadi zao za kisiasa, kidini, kijamii na jinsia, kuburudishwa na mechi za mpira wa miguu.

Katika miaka ya karibuni, kumekuwa na kukua kwa kiwango cha soka wilayani Ngara ambako kimekwenda sambamba na ongezeko la wapenzi na watazamaji wa mchezo huo na kupata mafanikio ya Timu za Murusagamba FC kuwa Mabingwa wa Mkoa wa Kagera 2015/2016 na Mabingwa wa sasa Kumuyange FC 2017/2018 huku Timu zake za soka zikinyanyasa vilivyo timu zingine za mkoa wa Kagera.

Hata hivyo, ongezeko hilo haliendi sanjari na ujenzi wa kiwanja hicho cha Kokoto au viwanja vipya pamoja na upanuzi na uboreshaji wa kuridhisha wa vile vilivyopo vya Kemikimba kilichopo mjini Benaco, Ule wa Kabanga uliopo Mjini Kabanga na ule wa Nazareth mjini Rulenge.
Rulenge Stars Mabingwa wa Polisi Jamii Cup 2018/2019 licha ya kupata ugumu katika uchezaji sababu ya ubora wa uwanja wa Kokoto lakini Timu huwa zinapambana kuonesha soka safi ili kupata matokeo mazuri dhidi ya wapinzani wao.

Aidha, Aprili 22 wakati akiwasilisha bungeni makadirio ya mapato na matumizi ya fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha 2016/2017, Majaliwa alisema serikali itaendelea kuimarisha michezo nchini ili kuwawezesha wanamichezo kufanya vizuri kitaifa na kimataifa.

“Kutokana na umuhimu wa michezo katika kuimarisha afya, kuongeza ajira, kujenga udugu na mshikamano miongoni mwa jamii na mataifa mbalimbali duniani, serikali itaendelea kuimarisha sekta hiyo kwa kusimamia maendeleo ya michezo katika shule, vyuo, taasisi na vilabu,” alisema kiongozi huyo wa serikali.

Majaliwa ambaye alitoa ahadi hiyo, ni kocha mwenye Leseni B ya Shirikisho la Soka Afrika (Caf).
Uchunguzi umebaini pia uwanja huu kutotoa fursa kwa Watazamaji  kukaa kwa raha na starehe wakati wa mechi pamoja na kukosa uzio madhubuti wa kuzuia watazamaji kuwafikia wachezaji na  waamuzi.


Je Halmashauri ya wilaya ya Ngara mnaufikiriaje uwanja huu wa Kokoto?? Ikiwa Serikali ya Awamu ya Tano ikiahidi kuinua michezo nchini??


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad