KUJINYONGA / UBAKAJI:- Mwanamke afariki Dunia baada ya kubakwa na kundi la Watu wasiojulikana Wilayani Ngara,mkoani Kagera. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, May 20, 2014

KUJINYONGA / UBAKAJI:- Mwanamke afariki Dunia baada ya kubakwa na kundi la Watu wasiojulikana Wilayani Ngara,mkoani Kagera.

Mwili wa marehemu Jenni  Furuguti  (60) ukiwa eneo la tukio, kitongoji cha Mukididili katika Mamlaka ya mji mdogo wa Ngara mkoani Kagera ukiwa umetelekezwa baada ya kufanyiwa tendo la ubakaji na watu wasiojulikana usiku wa kuamkia May 19,2014.

Jenni  Furuguti  (60) amefariki kutokana na Kubakwa na mtu zaidi ya mmoja ambapo mpaka wanafanya uchunguzi wamekuta sehemu za siri za marehemu zikitoka damu.

Mwanamke mmoja mkaziwa kitongoji cha Mukididili katika Mamlaka ya mji mdogo wa Ngara mkoani Kagera amekutwa amefariki dunia baada ya kufanyiwa tendo la ubakaji na watu wasiojulikana usiku wa kuamkia May 19,2014.

Kamanda wa jeshi la Polisi mkoani Kagera George Mayunga  amemtaja  mwanamke huyo  kuwa ni Jenni  Furuguti  (60) ambaye alikutwa jana(May 19,2014) jirani na eneo la  uwanja wa tenki la maji katika kitongoji hicho majira ya saa saba usiku. 

Kamanda Mayunga amesema  mwanamke huyo kabla ya kupatwa na mauti alikuwa katika starehe za kawaida kwa kupata kinywaji (pombe) na wakati anarejea nyumbani ndipo alikutana na watu hao na kumfanyia unyama huo. 

Ameongeza kuwa ,kutokana na  tukio hilo  tayari  mwanamke mmoja ambaye amekutwa na simu ya marehemu anashikiliwa na jeshi la Polisi wilayani Ngara kwa mahojiano zaidi kufuatia kifo hicho na uchunguzi unaendelea ili kubaini wahusika wengine.

Kamanda Mayunga amesema katika eneo la tukio kunaonyesha kuwa  kulikuwa na purukushani zilitokea na kwamba haikuwa rahisi kwa mwanamke huyo kujinasua na hivyo kubakwa ingawa katika sehemu ya mwili wake hapakuonesha michubuko ama majeraha. 

Aidha Taarifa za Daktari aliyeufanyia Uchunguzi mwili wa Marehemu,Dr.Daniel Dankani amesema kuwa ,Marehemu Jenni  Furuguti  (60)amefariki kutokana na Kubakwa na mtu zaidi ya mmoja ambapo mpaka wanafanya uchunguzi wamekuta sehemu za siri za marehemu zikitoka damu.

Wakati huo huo msichana mmoja  Furaha  Denis (16)aliyekuwa akifanya kazi za ndani  eneo la Ngara mjini   mkoani Kagera amejinyonga  hadi kufa  kwa kutumia kipande cha kanga nyumbani kwa mwajiri wake. 

Kaimu Mwenyekiti wa kitongoji cha  Ngara mjini  Thomas Milenzo  amesema msichana huyo ni mzaliwa wa kijiji cha Mabawe wilayani Ngara  na kwamba tukio hilo limetokea  May 17,2014,  majira ya saa 1 usiku nyumbani mwajiri wake ambaye ni Baruani Mbwana.

Jeshi la polisi Mkoani Kagera limethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba hilo ni tukio la nne kwa wilaya hiyo ndani ya mwezi huu wa tano la watu kujinyonga  na matukio mengine yanahusishwa na Imani za Ushirikina.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad