![]() |
ANFIELD. |
Katika
Dimba la ANFIELD jana Jumapili(Septemba
01,2013) ilishuhudia Liverpool ikishinda Bao 1-0 katika Mechi ya tatu mfululizo ya Ligi
Kuu Uingereza huku Mfungaji katika Mechi zote akiwa ni yule yule Daniel
Sturridge aliefunga Bao katika Dakika ya 4 tu na kuwaangusha Mabingwa watetezi
wa Uingereza Manchester United.
Aidha (Septemba 01) ni Bethdei ya Sturridge na Liverpool ndio wametimiza mwanzo wao mzuri kabisa katika Ligi kwa Miaka 19 na kuwafanya wawe kileleni mwa Ligi wakiwa na Pointi 9 kwa Mechi 3.
Bao
la Liverpool lilifungwa kufuatia Kona ambayo Beki wao Agger alipiga kichwa na
Mfungaji Sturridge kuuparaza Mpira wavuni.
Kwa
Man United, hii ikiwa Mechi yao ya 3 ya Ligi, wana Pointi 4 baada ya kushinda
moja, sare moja na kufungwa moja huku katika mchezo huo Man United walipata nafasi kadhaa zikiwemo
zile za Nani na Robin van Persie.
![]() |
Sturridge akiunanisha pasi ya Daniel Agger na ameifungia Liverpool katika mechi zote tatu msimu huu katika Ligi Kuu ya England, baada ya kuifunga Manchester United 1-0 Anfield. |
![]() |
Sturridge
akimkumbatia kocha wake Brendan Rodgers baada ya kufunga bao muhimu kwa
Liverpool.
|
![]() |
Gerrard
akipiga shuti la mpira wa adhabu ambalo liliokolewa na kipa David de Gea wakati
wa mchezo huo.
|
![]() |
Steven
Gerrard na Robin van Persie wakichimbiana mikwara wakati wa mchezo huo.
|
![]() |
Danny
Welbeck akienda chini baada ya kuchezewa rafu na Lucas na Iago Aspas
|
![]() |
Mshambuliaji
wa Liverpool, Luis Suarez anayetumikia adhabu alikuwepo Jukwaani akifatilia
mchezo huo ambao Liverpool walishinda bao 1-0 dhidi ya Manchester United.
|
![]() |
Makocha:
Kocha wa Liverpool, Rodgers (kulia) na wa Manchester United, David Moyes wakiwa
kazini katika mchezo huo.
|
Man
United walicheza Mechi hii bila ya Nyota wao Wayne Rooney ambae Mazoezini alipasuka Paji la Uso baada ya
kugongana na mwenziwe na inasemekana ameshonwa Nyuzi 10.
![]() |
Arsenal . |
Nao
Arsenal wameendeleza Rekodi yao murua ya kutofungwa Nyumbani na Mahasimu wao wa
London ya Kaskazini, Tottenham, baada ya kuwachapa Bao 1-0 katika Mechi ya Ligi Kuu na
hivyo kudumisha Rekodi ya kufungwa nao
mara moja tu tangu Mwaka 1993.
Tottenham
ilipokea kipigo chao cha kwanza cha Ligi Msimu huu kwa Bao la Dakika ya 23 la
Olivier Giroud baada kuunganisha krosi ya chini ya Theo Walcott na hilo ni Bao
lake la 4 Msimu huu.
Ushindi
huu umewafanya Arsenal wakamate Nafasi ya 4 kwenye Msimamo wa Ligi baada ya
kila Timu kucheza Mechi 3 na kuhakikisha Tottenham wameshinda mara moja toka
1993 Nyumbani kwa Arsenal.
LIGI
KUU ENGLAND RATIBA 2013/2014.
Jumamosi
14 Septemba,2013.
14:45
Manchester United v Crystal Palace
17:00
Aston Villa v Newcastle United
17:00
Fulham v West Bromwich Albion
17:00
Hull City v Cardiff City
17:00
Stoke City v Manchester City
17:00
Sunderland v Arsenal
17:00
Tottenham Hotspur v Norwich City
19:30
Everton v Chelsea
Jumapili
15 Septemba,2013.
18:00
Southampton v West Ham United
Jumatatu
16 Septemba,2013.
22:00
Swansea City v Liverpool
No comments:
Post a Comment