Kocha Moyes Mkosi Mtupu:- Man United yaburuzwa 3-1 na Sevilla. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, August 10, 2013

Kocha Moyes Mkosi Mtupu:- Man United yaburuzwa 3-1 na Sevilla.

Rio Ferdinand.
Katika Mechi Maalumu ya Kirafiki kumuenzi Beki wao Rio Ferdinand iliyochezwa Old Trafford na kuhudhuriwa na Watazamaji zaidi ya 50,000 Manchester United walifungwa Bao 3-1 na Sevilla ya Hispania.

Kabla Mechi hiyo kuanza, Rio Ferdinand, mwenye Miaka 34 na alietwaa Ubingwa wa Uingereza  mara 6 akiwa na Man United katika Misimu yake 11, aliwekewa Gwaride la Heshima na Wachezaji wa pande zote mbili na yeye aliingia Uwanjani akiwa na Watoto wake.


Sevilla walianza vizuri Mechi hii na kuleta kashikashi kubwa kwa Man United na hatimae kufunga Bao 2 za haraka zilizodumu hadi Mapumziko.

Kipindi cha Pili, Man United waliibuka na kucheza kwa kasi na kupata Bao kupitia Valencia kufuatia kazi nzuri ya Nyota Chipukizi Adnan Januzaj.

Mara baada ya kufunga Bao hilo, Valencia alitoa ishara ya mapenzi na kumshukuru Mungu kwa ajili ya Straika wa Nchi yao Ecuador, Chucho Benitez aliefariki huko Doha, Qatar Wiki iliyopita.

Baada ya hapo, Man United walikosa Goli baada ya Goli na mwishowe Sevilla wakapachika Bao la tatu.

MAGOLI.

Man United - 1

-Valencia Dakika ya 65.

Sevilla - 3

-Vitolo Dakika ya 21
-Marin 25
-Rabello 91

VIKOSI.

Man United: De Gea, Fabio, Ferdinand (Evans 82), Smalling, Buttner, Valencia (Carrick 65), Anderson (Giggs 65), Cleverley (Jones 46), Januzaj, Kagawa (Zaha 65), Henriquez (Lingard 46)

Akiba hawakucheza: Lindegaard, Bebe, M Keane.


Sevilla: Beto, Figueiras, Fazio, Pareja (Puerto 56), Alberto, Medel, Kondognbia, Marin, Perotti, Vitolo (Jairo 72), Bacca (Rabello 78).

Akiba hawakucheza: Julian, Navarro, Cala, Maduro, Guarente, Gameiro, Coke, Rusescu, Cotan.


Rio Ferdinand, akiwa na Watoto wake akiwapungia mkono mashabiki wa  Man United kabla ya kuanza kwa mechi na Sevilla.

Rio Ferdinand, mwenye Miaka 34, akiwapungia mkono mashabiki wa  Man United kabla ya kuanza kwa mechi na Sevilla.


Kocha mpya wa United, Moyes akisaini autographs wakati anaingia uwanjani.



Vitolo akifunga bao la kwanza dakika ya 21 pale Manchester United walifungwa Bao 3-1 na Sevilla ya Spain.



Ferdinand akiwa na Rais wa Sevilla FC, Jose Maria del Nido kabla ya mechi.
RIO FERDINAND-WASIFU:

JINA: Rio Gavin Ferdinand

KUZALIWA: 7 Novembar 1978, Denmark Hill, London, England

KLABU:

1992–1996   West Ham United [Timu ya Vijana]

1996–2000   West Ham United Mechi 127 Goli 2

1996–1997   Bournemouth (Mkopo) Mechi 10

2000–2002   Leeds United Mechi 54 Goli 2

2002– Manchester United Mechi 297 Goli 7

TIMU YA TAIFA:

1996–1997   England U-18         Mechi 7

1997–2000   England U-2 Mechi 15


1997–2011   England Mechi 81 Goli 3

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad