Arsenal walikosa Kombe lao wenyewe la Emirates Cup mbele ya Galatasaray kwa kuburuzwa 2-1 Nyumbani. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, August 05, 2013

Arsenal walikosa Kombe lao wenyewe la Emirates Cup mbele ya Galatasaray kwa kuburuzwa 2-1 Nyumbani.


Didier Drogba.
Mshambuliaji raia wa Ivory Coast, Didier Drogba ameendelea kuwa mwiba kwa Klabu ya Arsenal akikumbushia enzi zake alipokuwa na jezi ya Chelsea, baada ya mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 35  kufunga BAO mbili safi ndani ya Dakika 15 za mwisho, hapo jana(Agosti 04,2013) na kuiua Arsenal Nyumbani kwao Emirates na kulikosa Kombe lao wenyewe la Emirates Cup, baada ya Galatasaray ya Uturuki kutoka nyuma kwa Bao 0 -1 na kuifunga Arsenal Bao 2-1 na kutwaa Kombe hilo.

Katika Mechi  hiyo  Theo Walcott aliipa Bao Arsenal katika Dakika ya 39 na Drogba kusawazisha kwa Penati kwenye Dakika ya 79 na kufunga Bao la ushindi katika Dakika ya 87.

Awali FC Porto ya Ureno iliinyuka Napoli  ya Italia Bao 3-1 kwa Bao za Ghilas, Federico Fernandez aliejifunga mwenyewe na Lica huku Bao la Napoli likifungwa na Gorav Pandev kwa Penati.

MSIMAMO EMIRATES CUP 2013.

1 Galatasaray Pointi 6
2 FC Porto 3
3 Arsenal 1
4 Napoli 1

Drogba amefunga mabao dakika za lala salama Kombe la Emirates jana (Agosti 04,2013) kwa Penati kwenye Dakika ya 79 na kufunga Bao la ushindi katika Dakika ya 87.

Drogba akishangilia baada ya kufunga bao la pili kuiua Arsenal Nyumbani kwao Emirates na kulikosa Kombe lao wenyewe la Emirates Cup, baada ya Galatasaray ya Uturuki kushinda kwa Bao 2-1.



Yaya Sanogo aliyesajiliwa kutoka Klabu ya Ozere ya Ufaransa ameng'ara katika michuano yake ya kwanza ya Kombe la Emirates.

Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger alivyokuwa baada ya kipigo       na kulikosa Kombe lao wenyewe la Emirates Cup, baada ya Galatasaray ya Uturuki kushinda kwa Bao 2-1.

Emamanuel Eboue (kulia) alikuwa Nahodha wa Galatasaray ilipomenyana na timu yake ya zamani , Arsenal.

Walcott akishuhudia krosi yake ikiipa Arsenal bao la kuongoza katika mchezo wa kuwania kombe la Emirates 2013.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad