Yanga SC yaua 4-0 sasa wawa Pointi 3 mbele ya Timu ya Pili Azam FC na Pointi 8 mbele ya Timu ya 3, Simba SC ambao ndio Mabingwa watetezi wa Ligi kuu Vodacom Tanzania bara. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, February 13, 2013

Yanga SC yaua 4-0 sasa wawa Pointi 3 mbele ya Timu ya Pili Azam FC na Pointi 8 mbele ya Timu ya 3, Simba SC ambao ndio Mabingwa watetezi wa Ligi kuu Vodacom Tanzania bara.


Yanga SC
Vinara wa  Ligi Kuu Vodacom, Yanga SC  wameishushia kipigo Timu ya African Lyon  Bao 4-0 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kuzidi kujidhatiti  kileleni mwa Ligi hiyo kuu ya Soka Tanzania bara  wakiwa Pointi 3 mbele ya Timu ya Pili Azam FC na Pointi 8 mbele ya Timu ya 3, Simba SC  ambao ndio Mabingwa watetezi.


 

Kwa Matokeo hayo  yanaifanya Yanga SC  itimize pointi 36  baada ya kucheza mechi 16, ikiwazidi  Azam FC pointi  33  katika nafasi ya pili na mabingwa watetezi, Simba SC wanashika nafasi ya tatu kwa pointi zao 28.



Hadi mapumziko, Yanga SC  walikuwa tayari wanaongoza kwa mabao 2-0  ambayo yote yalitiwa kimiani na Jerry Tegete.



Hamisi Kiiza  alikosa penalti dakika ya 47 baada ya kipa Abdul Seif kudaka, kufuatia beki Ibrahim Job kumchezea rafu Haruna Niyonzima kwenye eneo la hatari. 



Didier Kavumbangu aliyeingia kuchukua nafasi ya Jery Tegete aliifungia Yanga bao la tatu kwa penalti dakika ya 69, baada ya beki Sunday Bakari kuunawa mpira kwenye mpira eneo la hatari.



Yanga ilihitimisha karamu yake mabao  kupitia kwa kiungo Nizar Khalfan aliyeingia kipindi cha pili pia kuchukua nafasi ya Simon Msuva, aliyefunga bao la nne dakika ya 80 kwa shuti akiunganisha krosi ya Saidi Bahanuzi, aliyetokea benchi pia kumpokea Kiiza.



Yussuf Mlipli alitolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 90, baada ya kumchezea rafu David Luhende. 



Katika mechi nyingine za Ligi kuu soka Tanzania bara, Toto African ilitoka 2-2 na Polisi Moro kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza wakati Mtibwa Sugar nayo imelazimishwa sare 0 – 0  na Ruvu Shooting kwenye Uwanja wa Manungu, Turiani, Morogoro.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad