Tazama Picha 2 kali za Muonekano wa Daraja la Kimataifa la Rusumo linalotumika kuunganisha nchi jirani za Rwanda na Tanzania. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, August 10, 2013

Tazama Picha 2 kali za Muonekano wa Daraja la Kimataifa la Rusumo linalotumika kuunganisha nchi jirani za Rwanda na Tanzania.

Kwa mbali ni  Muonekano wa Daraja la Kimataifa la Rusumo linalotumika kuunganisha nchi jirani za Rwanda na Tanzania na Ukivuka daraja hili upo nchi jirani ya Rwanda.



Haya ni  maji yenye Kasi ya Ajabu ya  Rusumo falls,tetesi  kubwa  ya kwamba  maongezi yapo ukingoni kwa nchi wahisani (Tanzania,Rwanda na Burundi) kuja kufua umeme na kuleta neema kwa Tanzania,Rwanda na Burundi maana mito ya nchi hizo ndio inaungana na kuleta hali hiyo ya Maporomoko  na hakika dalili za kupata umeme  zipo.


Ni  Daraja la Kimataifa la Rusumo linalotumika kuunganisha nchi jirani za Rwanda na Tanzania na Ukivuka daraja hili upo nchi jirani ya Rwanda.

Haya ni maporomoko ya maji yenye Kasi ya Ajabu ya  Rusumo falls,tetesi  kubwa  ya kwamba  maongezi yapo ukingoni kwa nchi wahisani (Tanzania,Rwanda na Burundi) kuja kufua umeme na kuleta neema kwa Tanzania,Rwanda na Burundi maana mito ya nchi hizo ndio inaungana na kuleta hali hiyo ya Maporomoko  na hakika dalili za kupata umeme  zipo.

Rusumo boda, mpakani mwa nchi jirani za Rwanda na Tanzania.

Rusumo boda, mpakani mwa nchi jirani za Rwanda na Tanzania.
Tayari  Serikali imesaini msaada wa shilingi bilioni 40 na serikali ya Japan kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa miradi miwili ya maendeleo hapa nchini.

Waziri wa Fedha na Uchumi Mustapha Mkulo amesema miradi hiyo ni ya ujenzi la wa daraja la Rusumo litakalounganisha nchi ya Tanzania na Rwanda na upanuzi wa barabara ya Kilwa ambapo itasaidia shughuli za maendeleo baina ya nchi hizo.

Pia Benki ya dunia kupitia bodi yake ya utendaji imeidhinisha dola Milioni 340 kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa uzalishaji wa umeme kwa kutumia nguvu za maji kwenye maporomoko ya mto Rusumo ulioko ukanda wa maziwa makuu barani Afrika.

Mradi huo unalenga kunufaisha wakazi Milioni 62 walioko Burundi, Rwanda na Tanzania na unafuatia ziara ya Rais wa Benki ya dunia Jim Yong Kim na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon kwenye ukanda huo mwezi Mei mwaka huu.

Colin Bruce ambaye ni Mkurugenzi wa mikakati na operesheni kwenye Benki ya dunia amesema kukamilika kwa mradi huo kutatoa hakikisho la upatikanaji wa umeme, kutapunguza gharama za umeme na kuchochea shughuli za kiuchumi zitakazowezesha kuongeza upatikanaji wa ajira.


Amesema uhaba wa umeme kwenye eneo hilo ni kikwazo kikubwa cha maendeleo ambapo ni asilimia nne tu ya wananchi wa Burundi wanapata huduma ya umeme ilhali Rwanda ni asilimia 13 na Tanzania ni asilimia 15.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad