Azam FC yashinda 1-0 dhidi ya Mamelodi Sundwons. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, August 07, 2013

Azam FC yashinda 1-0 dhidi ya Mamelodi Sundwons.

Bao pekee la Gaudence Exavery Mwaikimba jioni ya leo, limeipa ushindi wa 1-0 Azam FC ya Dar es Salaam katika mchezo wa kirafiki dhidi ya wenyeji Mamelodi Sundwons kwenye Uwanja wa mazoezi wa timu hiyo, uliopo Chloorkop, Johannesrbug Africa ya Kusini.

Huo ulikuwa mchezo wa pili kwa Azam FC katika ziara yao ya nchini hapa kujiandaa na msimu baada ya juzi kufungwa mabao 3-0 na Kaizer Chiefs.


Katika mchezo wa leo(Agosti 07,2013), hadi mapumziko hakuna timu iliyofanikiwa kuona lango la mwenzake na wenyeji ndiyo waliotawala zaidi mchezo kipindi hicho, ingawa Azam FC walifanikiwa kutengeneza nafasi nzuri zaidi ya kufunga.


Azam FC ilisafiri Jumamosi (03,2013) ya wiki iliyopita kuelekea afrika ya kusini kwa maandalizi ya ligi kuu na itacheza michezo minne kama ifuatavyo.

Tarehe 5 August, Azam Fc vs Kaizer Chiefs,

Tarehe 7 August Azam Fc vs Mamelodi Sundows,

Tarehe 9 August Azam Fc vs Orlando Pirates,

Tarehe 12 August Azam Fc vs Moroka Swalows.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad