Shirikisho
la Soka ukanda wa Africa Mashariki na Kati CECAFA limeichukua nchi ya Malawi badala ya Cameroun na Zimbabwe kama Timu ya Wageni waalikwa kuibadili nchini ya Djibouti katika michuano ya CECAFA
Tusker CHALENJI CUP 2012/2013
,mashindano yatakayoanza huko Nchini Uganda Novemba 24 na kumalizika Desemba 8
,mwaka huu.
Katibu
Mkuu wa CECAFA, Nicholas Musonye, amesema wameiteua Malawi kwa sababu katika
Mashindano mawili ya CHALENJI CUP yaliyopita Nchi hii imeonyesha Soka safi na
nidhamu ya hali ya juu.
Aidha
Droo ya kupanga Ratiba za Mashindano hayo imefanyika Mjini Kampala, nchini Uganda leo Novemba 12,mwaka huu.
Kundi A
Uganda
Kenya
Ethiopia
Sudani Kusini
Kundi B
Sudan Kaskazini
Sudan Kaskazini
Tanzania Bara
Burundi
Somalia
Kundi C
Rwanda
Zanzibar
Eritrea
Malawi
Tayari
Timu ya Somalia imeshawasili Nchini Uganda tangu Ijumaa iliyopita.
Wadhamini
wa Mashindano haya ni East African Breweries ambao wametoa Dola 450,000
kuendesha michuano hiyo huku Mshindi akipata $30,000, Mshindi wa Pili $20,000
na wa Mshindi wa Tatu ni $10,000.
Wakati
huo huo, Wenyeji wa CHALENJI CUP, Uganda, wametangaza Kikosi chao kwa ajili ya
michuano hiyo na miongoni mwao ni Mastraika hatari wa Ligi Kuu Vodacom, VPL,
Emmanuel Okwi wa Simba na Hamisi Kiiza wa Yanga.





No comments:
Post a Comment