
Felix
aliyeingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Mnigeria, Enyinna Darlington kwa
kumtungua bao hilo, kipa Mghana wa Yanga, Yaw Berko, ameendeleza rekodi yake
kuvifunga vigogo, Simba na Yanga katika Uwanja huo.
Hiyo
inakuwa mechi ya pili Yanga kufungwa ndani ya mechi sita walizocheza hadi sasa
na mbili wametoka sare- maana yake inabaki na pointi zake nane na kuzidi
kujipunguzia matumaini ya ubingwa msimu huu, ikiwa sasa inazidiwa pointi nane
na vinara wa ligi hiyo Simba SC.
Aidha,
hii ni mechi ya pili Yanga inacheza chini ya kocha wake mpya, Mholanzi Ernie
Blandts aliyerithi mikoba ya Mbelgiji, Tom Saintfiet na katika mechi hizo mbili
ameambulia pointi moja kutokana na sare dhidi ya Simba Jumatano.
Kwa
ujumla Yanga haijashinda hata mechi moja ya ugenini kati ya tatu ilizocheza
hadi sasa, ilitoka 0-0 na Prisons, ikafungwa 3-0 na Mtibwa na leo imechapwa 1-0
na Kagera Sugar, wakati Alhamisi itacheza na Toto African mjini Mwanza.
Katika
mechi hiyo, Yanga ilipata pigo dakika ya 23 baada ya mshambuliaji wake mahiri
na tegemeo, Said Bahanuzi ‘Spider Man’ kuchanika nyama za paja dakika ya 23,
baada ya kugongana na beki Benjamin Effe wa Kagera Sugar na kushindwa kuendelea
na mchezo, nafasi yake ikichukuliwa na Jerry Tegete.
Tangu
ajiunge na Yanga akitokea Mtibwa Sugar msimu huu, leo Bahanuzi amecheza mechi
ya 13 kwa dakika hizo 23 na ameifungia timu hiyo jumla ya mabao 12, matatu kati
ya hayo kwa penalti.

Katika
mechi hiyo iliyochezeshwa na refa Amon Paul wa Mara, aliyesaidiwa na Anold
Bugabo wa Singida na Charles Simon wa Dodoma, hadi mapumziko Simba walikuwa
tayari mbele kwa mabao 2-1, mabao yake yote yakitiwa kimiani na kiungo Amri
Ramadhan Kiemba katika dakika za 16 na 44, wakati la Oljoro lilifungwa na Paul
Nonga dakika ya 29.
Kiemba
alifunga bao la kwanza akiunganisha krosi pasi ya Christopher Edward, wakati
bao la pili lilitokana na krosi ya Nassor Masoud ‘Chollo’, yote kutokana na
mashambulizi ya upande wa kulia.
Kwa
ushindi huo, Simba imefikisha pointi 16 baada ya kucheza mechi sita, hivyo
kuendelea kuongoza Ligi Kuu, ikifuatiwa na Azam yenye pointi 13, ingawa
imecheza mechi tano.
Katika
mechi nyingine za jana, Mgambo imepata ushindi wake wa kwanza baada ya kuichapa
Polisi Morogoro 1-0, wakati Toto African imeichapa JKT Ruvu 2-1 na Prisons
imelazimishwa sare ya bila kufungana na Mtibwa Sugar.
No comments:
Post a Comment