Watu wawili
wamefariki Dunia wilayani Kasulu mkoani Kigoma kufuatia ajali ya gari la Mkurugenzi
Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania TBC Dkt. Ayub Rioba, lililokuwa
likitokea wilayani Kibondo kwenda Kigoma Mjini.
Kamanda wa
Jeshi la Polisi mkoa wa Kigoma, Kamishna Msaidizi Martin Otieno amethibitisha
kutokea kwa ajali hiyo na kusema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni utelezi
uliosababisha gari kuacha njia na kuwagonga waenda kwa miguu watatu.
Kamanda Otieno aliwataja waliofariki katika ajali
hiyo kuwa ni watembea kwa miguu wawili, waliofahamika kwa majina ya Teresia
Mpoma (55) mkulima na Mkazi wa Nyakitonto, Yuster Masharubu (55) mkazi wa
Nyakitonto na Majeruhi mmoja aliefahamika kwa jina la Diana Shedrack (10)
mwanafunzi shule ya Msingi Nyakitonto, ambae hali yake ilielezwa kuwa mbaya
huku akiendelea na matibabu katika Hospitali ya Wilaya ya Kasulu.
Amesmea Gari
la Mkurugenzi Mkuu wa TBC lililopata ajali lenye namba za usajili STK 8769
lilikuwa na abiria wawili akiwemo mkurugenzi mkuu wa TBC, Dkt. Ayub Rioba na
Mkuu wa kanda ya magharibi TBC Mhandisi Zebron Mafuru ambao wote wametoka
salama na hali zao ni nzuri.
Kamanda
Otieno aliongeza kwwa kutoa tahadhari kufuatia
Chanzo cha ajali hiyo kuwa ni utelezi unaotokana na Mvua zinazoendelea
kunyesha Katika Mkoa huo,hivyo amewaomba madereva kuendesha magari kwa umakini
kutokana na ubovu wa barabara hiyo na kuzingatia sheria za barabarani.
Dkt. Rioba
yuko katika ziara ya kukagua vituo vipya vya matangazo vilivyojengwa katika
maeneo ya mipakani.
|
No comments:
Post a Comment