Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Prof Joyce Ndalichako
pamoja na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ,Injinia Hamad Masauni
wakimfariji Mama Mzazi wa marehemu Aqwilina jioni ya leo Mbezi Kimara
jijini Dar.
Mwanafunzi
huyo wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji(NIT) amepoteza maisha baada ya kupigwa
risasi Februari 16 mwaka huu eneo la Mkwajuni jijini Dar es Salaam wakati
Polisi walipokuwa wakizuia maandamano ya chama cha CHADEMA.Kufuatia kifo cha
Mwanafunzi huyo Serikali imesema itabeba jukumu la Mazishi yake.
Aidha Rais
Dkt John Pombe Magufuli amesema amesikitishwa sana na kifo cha mwanafunzi
huyo,Aqwilina Akwilini wa Chuo cha Usafirishaji (NIT).
"Natoa
pole kwa familia,ndugu,wanafunzi wa NIT na wote walioguswa na msiba
huu.Nimeviagiza vyombo vya dola kufanya uchunguzi na kuwachukulia hatua za
kisheria waliosababisha tukio hili",Ilisema sehemu ya taarifa yake iliyotolewa mapema leo february 18,2018.
Waziri wa
Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Prof Joyce Ndalichako (tatu kulia)
akiwafariji Mama Mzazi wa marehemu Aqwilina pamoja na ndugu jioni ya leo
Mbezi Kimara jijini Dar es Salaam.
Mama wa
Marehemu Akwiline akilia kwa uchungu mara baada ya kuona viongozi wa Waandamizi
wa serikali walipofika nyumbani kwake,Mbezi Kimara jioni ya leo kwa lengo la
kutoa pole na kufahamu taratibu mbalimbali za msiba huo.
No comments:
Post a Comment