Rais
Magufuli amesema alipoingia madarakani alikuta changamoto nyingi zikiwemo za
wafanyakazi hewa, vyeti feki na ufisadi.
Amesema
baada ya kudhibiti, watumishi wa umma 12,000 wamepatikana na vyeti feki
wakiwemo walimu 3,655 tangu walipoanza kuhakiki.
Amesema
uhakiki huo ulibaini watumishi hewa 20,000 na kwamba, Serikali ilikuwa
inapoteza fedha nyingi kuwalipa mishahara.
“Kila kitu
kilikuwa hewa hata mapenzi inawezekana yalikuwa hewa,” amesema Rais Magufuli.
|
Amesema
kutokana na udhibiti wa fedha za Serikali ni lazima watu waliokuwa wanapata
fedha kwa njia zisizo halali watalalamika kuwa vyuma vimekaza.
Kuhusu madai
ya walimu, amesema Sh25 bilioni wanazoidai Serikali zitalipwa baada ya uhakiki
kumalizika.
|
No comments:
Post a Comment