Rais Dk. John Magufuli akipokelewa na Jakaya
Kikwete.
RAIS Dk.
John Magufuli amefanya mambo mengi ndani ya mwaka huu, lakini haya 10 yatazidi
kukumbukwa na Watanzania.
BABU
SEYA, PAPII KOCHA.
Tukio la
kuachiwa kwa wanamuziki Nguza Mbangu Viking (Babu Seya) na Johnson Nguza (Papii
Kocha) lilitangazwa na Rais Magufuli wakati wa maadhimisho ya uhuru, Desemba 9,
mwaka huu.
Rais
alipotangaza msamaha kwa wanamuziki hao maarufu kuliamsha nderemo na vifijo
kutoka kwa mashabiki wa muziki wa dansi nchini.
Familia hiyo
ilianza kutumikia kifungo cha maisha jela tangu Juni mwaka 2004 kwa kosa la
kuwalati wanafunzi wa Shule ya Msingi Mashujaa, jijini Dar es Salaam.
RELI YA
KISASA.
Tukio la
ujenzi wa reli ya kisasa lilikuwa la kipekee kwa nchi yetu kwani Rais Magufuli
alizindua rasmi ujenzi wake akasema itasafiri kwa mwendo wa kilomita 160 kwa
saa.
Rais alisema
Tanzania ndiyo nchi pekee barani Afrika ambayo imeweza kujenga mradi wa reli
kama hiyo kwa fedha zake za ndani.
Ujenzi wake
umeanzia Dar es Salaam kwenda Morogoro na utagharimu dola za Marekani bilioni
1.29 na shughuli za ujenzi wa reli hiyo zinaendelea.
TANESCO,
WIZARA ZIVUNJWE.
Mwaka huu
pia, Rais Magufuli alitembelea mradi wa ujenzi wa barabara za juu eneo la
Ubungo na kuagiza majengo ya makao makuu ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco)
na Wizara ya Maji yavunjwe.
Alitoa
maagizo hayo kutokana na majengo hayo kujengwa ndani ya hifadhi ya barabara ya
Morogoro.
Majengo ya
wizara tayari yamevunjwa na Tanesco inaendelea na mchakato wa ubomoaji.
|
MABWENI YA UDSM.
Jambo
jingine ambalo Rais Magufuli atakumbukwa nalo kwa mwaka huu, ni uzinduzi wa
majengo mapya ya mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM).
Mabweni hayo
yana uwezo wa kuchukua wanafunzi 3,840 na yalijengwa chini ya mwaka mmoja na
kugharimu sh. bilioni 10.
Hivi
karibuni majengo hayo yaliripotiwa kuwa na nyufa, lakini Wakala wa Majengo
Tanzania (TBA) uliwatoa hofu wanafunzi kuwa hayana tatizo.
KUVUNJA
BARAZA LA MAWAZIRI.
Oktoba mwaka
huu, Rais Magufuli alivunja Baraza la Mawaziri na kufanya mabadiliko kadhaa.
Katika
mabadiliko hayo, aliongeza wizara na mawaziri kutoka 19 hadi 21. Nafasi za
manaibu mawaziri ziliongezwa kutoka 16 hadi 21.
Lengo la
mabadiliko hayo ilielezwa ni kuleta ufanisi wa kiutendaji serikalini.
DAWA ZA
KULEVYA.
Alipoingia
madarakani alitangaza kiama cha wauzaji na watumiaji wa dawa za kulevya na
vigogo kadhaa walikamatwa kujihusisha nazo.
Februari
mwaka huu, rais alimteua Rogers Sianga kuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia
na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA).
Baada ya
uteuzi huo, Sianga alimhakikishia rais kuwa atapambana na dawa hizo hadi
ushindi upatikane.
Agosti,
mwaka huu, Rais Magufuli alimteua pia Luteni Kanali Frederick Felix Milanzi
kuwa Kamishna wa Operesheni wa mamlaka hiyo ili kukoleza vizuri moto wa
kukabiliana na dawa hizo nchini.
BANDARINI.
Mwaka huu
rais alifanya pia ziara ya kushtukiza bandarini na kukuta tena madudu mengine,
ikiwa ni mwendelezo wa ziara zake bandarini hapo.
Safari hii
alikuta magari 50 yaliyoagizwa nchini na watu wasiojulikana kwa jina la Ofisi
ya Rais.
Rais
Magufuli alisema magari hayo siri yake ni kubwa kwani yamekaa bandarini tangu
Juni mwaka 2015 na yaliletwa pamoja na magari ya serikali.
Akahoji,“inakuwaje
rais nipate taarifa za magari kufichwa lakini waziri, Mamlaka ya Mapato
Tanzania (TRA), Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) msijue?”
|
MADENI YA
WALIMU.
Desemba
mwaka huu, rais alirejesha matumani ya walimu ambao kwa muda mrefu wanasumbukia
madai yao bila ufumbuzi.
Akizungumza
na mamia ya wanachama wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Desemba 14, mwaka
huu, mjini Dodoma, aliahidi kulipa takriban sh. bilioni 25 za madeni ya walimu.
“Ninawaahidi
walimu wenzangu, mara baada ya uhakiki kuisha wale walimu ambao wanadai malipo
halali watalipwa,”alisema.
Alisema
kabla hajawa rais alikuwa mwalimu hivyo anazifahamu vizuri shida za walimu
hivyo walimu wajisikie wana mwakilishi mzuri.
MADINI.
Rais
Magufuli aliunda tume mbili kuchunguza madai ya wizi na ufisadi unaodaiwa
kufanywa na wawekezaji tangu walipoanza uzalishaji wa dhahabu nchini.
Ripoti ya
kamati ya kwanza ilipotoka ikiongozwa na Profesa Abdulkarim Mruma ilibaini
kasoro za usimamiaji, hivyo rais alimfuta kazi Waziri wa Nishati na Madini,
Profesa Sospeter Muhongo na kuvunja Bodi ya Uwakala wa Ukaguzi wa Madini
Tanzania (TMAA).
Ripoti ya
kamati ya pili iliongozwa na Profesa Nehemia Ossoro ilibaini usafirishaji wa
mchanga umepotezea taifa fedha nyingi.
Profesa
Ossoro alisema fedha zilizopotea tangu mwaka 1998 ni kati ya sh. trilioni 132
hadi trilioni 380.
BOMBA LA
MAFUTA.
Mwaka huu
ulikuwa pia na tukio la aina yake. Ni uzinduzi wa ujenzi wa bomba la mafuta
ghafi kutoka Hoima Uganda hadi Bandari ya Tanga.
Bomba
litapita mikoa nane, wilaya 24 na vijiji 124 na wakandarasi watatu kutoka nje
wanasimamia mradi huo na kutoa fursa mbalimbali za ajira kwa wananchi wa pande
hizo mbili.
NA JULIAN
MSACKY
|
No comments:
Post a Comment