Maelfu ya
raia wa Zimbabwe jana walijitokeza barabarani hasa mjini Harare katika jitihada
za kuongeza shinikizo za kumtaka rais Mugabe ajiuzuulu.
Rais Mugabe
anatarajiwa kukutana na viongozi wa jeshi la nchi hiyo na tayari msafara wa
magari umeonekana ukitoka nyumbani kwake.
Kiongozi wa
chama cha maveterani wa vita ya ukombozi wa Taifa hilo, Chris Mutsvangwa
ameliambia Shirika la Habari la Reuters kwamba, chama hicho pia kimeanza
mchakato wa kumwondoa Mugabe kama Rais wa nchi hiyo.
Reuters
imeripoti kwamba Grace, mkewe Mugabe amefukuzwa uanachama.
Watu
wameonekana mitaani wakicheza na kushangilia baada ya ZANU PF kumwondoa katika
uongozi Mugabe.
|
Sunday, November 19, 2017
Rais Mugabe Avuliwa Uongozi Ndani ya ZANU PF.
Tags
# SIASA
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
SIASA
Labels:
SIASA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
No comments:
Post a Comment