John Bocco
ameipa Simba SC ushindi wa kwanza dhidi ya Tanzania Prisons tangu iliposhinda mara
ya mwisho 2013 kwenye uwanja wa Sokoine Mbeya.
Bao pekee la
ushindi limefungwa dakika ya 84 kipindi cha pili baada ya Bocco kuuwahi mpira
uliochelewa kuokolewa na mabeki wa Tanzania Prisons.
Simba
SC imepata pointi sita kwenye uwanja wa Sokoine baada ya kusubiri kwa muda mrefu.
Ushindi huo unaifanya Simba SC ifikishe pointi 22 ikiwa inaongoza ligi mbele ya
Azam FC ambayo itacheza kesho dhidi ya Njombe Mji FC.
Yanga SC
inabaki katika nafasi ya tatu huku Mtibwa Sugar ikiwa nafasi ya nne timu zote
zikiwa na pointi 17 lakini zinatofautiana kwa wastani wa magoli. (Azam FC , Yanga
SC na Mtibwa Sugar ni timu tatu ambazo zipo nafasi Nne za juu zikiifukuza Simba SC kileleni
kwenye msimamo wa VPL 2017/2018).
Matokeo
ya mechi nyingine zilizochezwa leo Jumamosi Nov 18, 2017.
|
No comments:
Post a Comment