Waziri wa
Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe.
Selemani S. Jafo (Mb) amesema jumla ya watumishi wa Sekta ya Afya wapatao 2058
wamekwisha pangiwa vituo vya kazi kuanzia leo 06/11/2017 na taarifa zote
zinapatikana kwenye mtandao wa Ofisi ya Rais TAMISEMI.
“Taarifa ya
watumishi 2058 imekamilika na itarushwa kwenye mtandao wa OR TAMISEMI leo
tarehe 6/11/2017 jioni, hivyo Makatibu Tawala wa Mikoa na Wakurugenzi wa
Halmashauri zote nchini wanatakiwa kujiandaa kuwapokea watumishi hao ikiwemo
kuwapatia stahiki zao”
Amewataka
Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa na Waajiri kuhakikisha wanachukua
taarifa za watumishi walioripoti na kuwaingiza kwenye Mfumo wa Mishahara na
kuwapangia katika maeneo ambayo ya uhitaji mkubwa ili kuboresha huduma za afya
nchini.
Pia ameekeza
watumishi wanaopangiwa vituo, kuripoti katika vituo vyao vya kazi ndani ya siku
14 tangu tangazo hili kutolewa.
Aidha,
Waajiri wote watoe taarifa juu ya kuripoti kwa watumishio haa wapya na vituo
walivyopangiwa siku 14 baada ya kuripoti kwao.
Taarifa za
Watumishi hao na Vituo vyao vya kazi, inapatikana katika Mtandao wa Ofisi ya
Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR TAMISEMI) wa www.tamisemi.go.tz.
AU BOFYA HAPA CHINI KUSOMA JINA LAKO.
No comments:
Post a Comment