Simba SC ina
nafasi kubwa ya kuharibu hesabu za Mtibwa Sugar ikishinda mchezo wa kesho September
21,2017 dhidi ya Mbao FC kwa kuiondoa kileleni mwa msimamo wa ligi kuu ya
Vodacom Tanzania bara 2017/2018 utakaofanyika kwenye uwanja wa CCM Kirumba
jijini Mwanza.
Simba SC ambayo
kwa sasa ina pointi 7 ikiibuka na ushindi kwenye mchezo huo itafikisha alama 10
na kuishusha kileleni Mtibwa Sugar yenye pointi 9 ikiwa imecheza mechi tatu.
Tayari Simba
SC imecheza mechi tatu za Ligi Kuu msimu huu, ikishinda mechi mbili kwa bao 7-0 dhidi ya Ruvu
Shooting na 3-0 dhidi ya Mwadui FC Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam, wakati
mwingine wametoka sare ta 0-0 na Azam FC Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es
Salaam.
Katika mabao
10 iliyovuna kwenye mechi mbili, mshambuliaji Mganda, Emmanuel Okwi amefunga
mabao sita, manne dhidi ya Ruvu na mawili dhidi ya Mwadui, sasa akiwa anaongoza
kwa kufunga katika Ligi Kuu.
|
No comments:
Post a Comment