Mbunge wa
Iringa Mjini (CHADEMA) Petter Msigwa ameachiwa huru Jana,September 24,2017, usiku kwa dhamana baada
ya kukamatwa akiwa kwenye mkutano wa hadhara.
Msigwa
aliachiwa baada ya kudhaminiwa na wadhamini wawili Alex Kimbe pamoja na
Mwenyekiti wa BAVICHA- Iringa Leonce Marto , saa nne usiku .
Msigwa
alishushwa Jukwaani kwa nguvu akiwa anahutubia mkutano wa hadhara
katika kata ya Mlandege Manispaa ya Iringa na anatuhumiwa kwa kosa la uchochezi
dhidi ya vyombo vya usalama .
Marto
amesema mikutano yake imefungiwa na hapaswi kuendelea na ziara yake
katika kata nyingine mpaka hapo OCD atakapo amua vinginevyo.
Leo,Jumatatu September 25,2017,
Mbunge anatakiwa kuripoti kwa RCO na huenda kesi ya uchochezi ambayo tayari
imeshafunguliwa jalada lake ikapelekwa mahakamani .
Amesema
Mbunge huyo atazungumza na vyombo vya habari leo mchana kuweka wazi
madhila yaliyompata wakati akitekeleza wajibu wake kwa wananchi.
|
No comments:
Post a Comment