Rais Magufuli asema Serikali itaifanyia Matengenezo barabara ya Nyakahura – Rusumo – Ngara. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, July 19, 2017

Rais Magufuli asema Serikali itaifanyia Matengenezo barabara ya Nyakahura – Rusumo – Ngara.

Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akihutubia wa wananchi kijiji cha Nyakahura waliokuwa njiani kumpokea akiwa njiani akielekea Ngara Mkoani Kagera, 19 Julai 2017. Picha na Ikulu.

Akiwa njiani kuelekea Ngara, Mhe. Rais Magufuli amesimamishwa na wananchi wa Nyakahura ambapo amewahakikishia kuwa Serikali itaifanyia matengenezo ya barabara ya Nyakahura – Rusumo – Ngara, ameahidi kumtuma Waziri wa Maji na Umwagiliaji kwenda kuangalia namna ya kutatua tatizo la maji na pia amechangia Shilingi Milioni 10 katika ujenzi wa majengo ya shule. 
 
Kesho Alhamisi, tarehe 20 Julai, 2017 Mhe. Rais Magufuli ataendelea na ziara yake Mkoani Kagera ambapo hapa Ngara atazungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara utakaofanyika mchana.

Umati Waananchi waliohudhuria uzinduzi wa Biharamulo, Kagoma, Lusaunga yenye urefu wa kilometa 154,wakimshangilia,Mh Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli, mara baada ya kuwahutubia kwenye mkutano wa hadhara wa ufunguzi wa barabara kwenye viwanja vya stendi ya Biharamulo 19 Julai 2017.

Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli, akipungia vikundi vya kwaya,ngoma na Burudani alipowasili kwenye viwanja vya stendi ya Biharamulo tayari kwa kuzindua Barabara ya Biharamulo, Kagoma, Lusaunga yenye urefu wa kilometa 154,Biharamulo Mkoani Kagera wakati akiwa kwenye ziara ya siku mbili mkoani humo, 19 Julai 2017.

Barabara hiyo  imejengwa kwa gharama ya Shilingi Bilioni 190.4 zilizotolewa na Serikali ya Tanzania.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad