Rais Dkt. John Magufuli yupo kwenye ziara katika mikoa ya Kagera, Kigoma,Tabora na Singida ambako atafungua na kuzindua miradi 9 na Akizindua ujenzi wa barabara hiyo, Rais John Magufuli amesema kwamba Biharamulo imeshika nafasi ya pili kwa umaskini na wananchi wanafanya ulinganisho na hali ilivyo tofauti katika wilaya jirani ya Chato. |
Rais
akiwapungia mkono wananchi wa Biharamulo.
Katika hatua Nyingine, Rais John
Magufuli ametoa siku 14 kwa wamiliki wa vituo vya mafuta kote nchini kutumia
mashine stahiki za risiti za kielektroniki (EFDs) huku akisisitiza kuwa
watakaoshindwa watafutiwa leseni zao.
Hivi karibuni, Waziri wa Fedha na Mipango, Prof.
Philip Mpango alivifungia baadhi ya
vituo vya mafuta hapa nchini baada ya kubainika kuwa vilikuwa havitumii mashine
stahiki za EFDs.
|
Rais
akisalimiana na Wazee wa Biharamulo.
Kwa upande
wake Mbunge wa Biharamulo, Oscar Mukasa amesema wanaunga mkono msimamo wa Rais
kupiga marufuku wanafunzi wanaobeba mimba kuendelea na masomo na wameanzisha
shule ya wasichana ya bweni kuunga mkono kauli yake.
|
No comments:
Post a Comment