Jamal
Malinzi na Mwesigwa wakifikishwa Mahakamani leo.
Rais wa
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amerejeshwa rumande kwa siku
nyingine 11 baada ya kesi inayomkabili ya kugushi nyaraka na kutakatisha fedha
kushindwa kuanza kusikilizwa kutokana na upepezi kutokamilika.
Malinzi
anayetuhumiwa na mashtaka 28 tofauti pamoja na Katibu Mkuu wa TFF, Celestine
Mwesigwa na Mtunza Fedha, Nsiande Mwanga wanaokabiliwa na mashtaka matatu,
wamepandishwa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo Jumatatu, Julai 31,
asubuhi, chini ya Hakimu Mkazi Mkuu, Willbroad Mashauri, lakini kesi hiyo
haikuweza kusikilizwa.
Mawakili wa
upande wa Jamhuri ambao ndiyo walalamikaji, waliiambia Mahakama kwamba
upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika, hivyo washtakiwa hao kurejeshwa
rumande hadi Agosti 11,2017.
Awali,
Malinzi na wenzake walisomewa mashtaka hayo ya kughushi nyaraka na kutakatisha
fedha, Juni 29 mwaka huu, na kupelekwa rumande kutokana na kesi hiyo kutokuwa
na dhamana na sasa wataendelea kusubiri kwa wiki hizo mbili.
NA DENIS MTIMA
|
No comments:
Post a Comment