Kamanda Mkuu
wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP), Simon Sirro.
Kamanda Mkuu
wa Jeshi la Polisi (IGP), Simon Sirro ametoa agizo kuwa mchakato ufanyike wa
kuzivunja timu zote za jeshi la polisi zinazoshiriki ligi za soka za madaraja
tofauti ili iundwe timu moja.
Kamanda Sirro
amesema kuwa hatua hiyo itachukuliwa ili kuifanya timu moja ambayo itaundwa iwe
na nguvu na kuwe na maandalizi mazuri kuliko ilivyo sasa ambapo kuna timu
nyingi lakini hazifanyi vizuri.
IGP Sirro
amesema amesisitiza kuwa ameshatoa mwongozo kwa kamishna wa idara husika ili
mchakato wa kuzifuta timu zilizopo katika madaraja tofauti ufanyike kwa faida
ya kulipa jeshi nguvu liwe na timu moja imara.
Timu hiyo
ambayo itaundwa itafahamika kwa jina kla Polisi Tanzania na itakuwa inachukua
wachezaji wenye vipaji vya juu kutoka katika vituo mbalimbali vya jeshi la
polisi.
Kuhusu
michezo mingine, IGP Sirro amesema inafanyika lakini vijana wake wanahitaji
motisha ili waweze kuonekana, na kusisitiza kuwa hilo litafanyika ili kuboresha
michezo mingine ikiwemo ndondi, mieleka na judo.
|
No comments:
Post a Comment