“Ni lazima
ufanye mabadiliko makubwa, nataka kuona Jeshi la Polisi linakuwa Jeshi la
Polisi, Wewe IGP Sirro na Makamnda wenzako hakikisheni mnakomesha uhalifu,
komesheni mauaji dhidi ya raia, ujambazi na dawa za kulevya” amesema Mhe. Rais
Magufuli.
Aidha, Mhe. Rais Magufuli amewataka Makamanda, Maofisana Askari wa jeshi hilo kujiepusha na rushwa, dawa za kulevya, kutumiwa na watu kwa maslai binafsi, kuingia mikataba isiyo na maslai kwa Jeshi na Taifa, ubadhirifu na kuacha upendeleo katika utoaji wa ajira na vyeo. Mhe. Rais Magufuli pia ametaka Makamanda, Maofisa na Askari wote wa Jeshi la Polisi wampe ushirikiano wa kutosha IGP Simon Sirro ambaye hivi karibuni amemteua kuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini. Kikao hicho kimehudhuriwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Meja Jenerali Mstaafu Projest Rwegasira. Gerson Msigwa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU Dar es Salaam 02 Juni, 2017 |
Friday, June 02, 2017
Yafahamu Maagizo Mazito ya Rais Magufuli kwa IGP Simon Sirro Leo June 2, 2017.
Tags
# HABARI
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
HABARI
Labels:
HABARI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
No comments:
Post a Comment