Mbunge wa
Jimbo la Kibamba, Mhe. John Mnyika leo
June 2, 2017 alisababisha kuzaazaa Bungeni Dodoma baada ya kugoma
kutoka nje ya Bunge alipoamuriwa na Spika Job Ndugai kutokana na kile
kilichodaiwa kukataa kuketi kama alivyoamuriwa na kiongozi huyo wakati mijadala
ikiendelea.
Chokochoko hizo ziliibuka baada ya
Mbunge wa Mvumi, Mhe.Livingstone Lusinde kudai kwamba
wapinzani bungeni humo wanatetea wezi wa mchanga wa dhahabu.
Mhe.Mnyika ilibidi asimame na kutoa mwongozo kwa kusema wao wapinzani
sio wezi isipokuwa walichokuwa wakikisema ni kulalamikia mikataba mibovu ya
madini ambayo imeingiwa na serikali na kusababisha kufikia hapa tulipo.
Wakati Mhe.Mnyika
akiendelea kumpa taarifa Lusinde, mbunge ambaye hajajulikana jina alisikika
akisema kwa sauti ‘mwizi’, hali iliyomfanya Mnyika kumuomba spika amjuwe
aliyemuita mwizi, hata hivyo, Spika Ndugai akawa anamsisitizia akae chini.
Alimuomba kukaa chini mara tatu
lakini Mnyika hakutii ndipo Ndugai alipomuamuru atoke nje lakini pia hakutoka,
hivyo akawaita askari wa bunge aliowaamuru waingie ndani na kumtoa nje kwa
nguvu mbunge huyo kijana.
Kuona hivyo Mbunge wa Kawe, Mhe.Halima
Mdee na yule wa Bunda, Mhe.Ester Bulaya, waliingilia kati kuwazuia
askari wa bunge kumtoa nje Mnyika, hali iliyoleta tafrani, hata hivyo,
alitolewa na kwenye lango la kuingilia bungeni, alisukumwa na ‘kutupwa’ nje ya
mjengo.
Spika alitangaza kumsimamisha Mhe.Mnyika
asihudhurie vikao vya bunge kwa wiki moja huku Mhe.Ester Bulaya na Mhe.Halima
Mdee akisema wataandikiwa barua ili wakahojiwe na Kamati ya Haki na Maadili
ya Bunge.
TAZAMA VIDEO YA TIMBWILI
HILO BUNGENI.
|
No comments:
Post a Comment