Kwenye Mechi
ya Kwanza, Timu Mpya ya Ligi Kuu Vodacom, Singida United, inayoongozwa na Kocha
wa zamani wa Yanga SC, Hans van der Pluijm, ilitangulia kufunga Bao Dakika ya 20
kupitia Pro wao kutoka Zimbabwe Kutinyu Tafadzwa.
Lakini AFC
Leopards walisawazisha Dakika ya 63 kupitia Vincent Oburu.
Hadi Dakika
90 kwisha Gemu ilibaki 1-1 na ikaja Tombola ya Mikwaju Mitano ya Penati ambapo
AFC Leopards walifuzu kwa Penati 5-4.
Baada ya
Mechi hii wakaingia Yanga SC ambao walitoka 0-0 na Tusker FC ya Kenya lakini
kufuzu kwa Penati 4-2 .
|
Tusker FC
walifunga Penati 2 wakati moja ikiokolewa na Kipa Deogratius Munishi ‘Dida’ na
nyingine kutoka nje baada kuparaza Posti.
RATIBA.
Jumanne Juni 6,2017
Saa 8 Mchana
Simba v Nakuru All Stars
Saa 10 na
Robo Jioni Gor Mahia v Jang’ombe Boys
Alhamisi Juni 8,2017.
Nusu Fainali
Saa 8 Mchana
AFC Leopards v Yanga
Saa 10 na
Robo Jioni Mshindi RF3 v Mshibdi RF 4
Jumapili Juni 11,2017.
Fainali
Saa 10 Jioni
|
No comments:
Post a Comment