Hii ni mara
ya 12 kwa Real Madrid kuwa Mabingwa wa Ulaya.
Kwa
Juventus,ya Italia ambao wameshinda Fainali zao mbili tu kati ya Nane walizotinga, sasa
wamefungwa katika zote Tano walizofika mara ya mwisho ambazo ni za Miaka ya
1997, 1998, 2003, 2015 na hii ya 2017.
Tangu AC
Milan wafanikiwe kutetea Ubingwa wa Ulaya Miaka ya 1989 na 1990, wakati huo
Kombe hili likiitwa, EUROPAEN CUP, hakuna Timu iliyowahi kutetea Taji hili la
UEFA Champions League hadi hii fainali ya Jana June 3, 2017 na Real Madrid
kuweka Historia hii.
|
Kwa Mchezaji
Bora Duniani sasa amefikisha Maba 105 ya Champions League na Msimu huu wa
2016/2017 ni Cristiano Ronaldo ndie
Mfungaji Bora wa Mashindano haya akiwa na Bao 12 akimpiku Lionel Messi wa FC Barcelona aliefunga Bao 11.
|
Mchezaji Cristiano
Ronaldo ameshinda Kombe la Klabu Bingwa Ulaya mara Nne sasa - mara tatu akiwa na
Real Madrid na Moja akiwa na Manchester United.
|
Mreno Cristiano Ronaldo alifunga mabao
mawili, la kwanza kwake na klabu dakika ya 20 na lake la pili dakika ya 64
kutoka kwa krosi ya Luka Modric.
Casemiro aliwafungia Real bao lao la pili
dakika ya 61 kabla ya Marco Asensio
kukamilisha ushindi wao dakika ya 90 kwa bao lao la nne.
|
Juventus,
waliokuwa wameanza vyema mechi hiyo wakikuwa wamekomboa bao la kwanza la Ronaldo dakika ya 27 kupitia Mario Mandzukic na kufanya mambo kuwa
sare wakati wa mapumziko lakini kipindi cha pili mawimbi yaliwageuka.
|
Real Madrid
wamefanikiwa kuwa klabu ya kwanza tangu AC Milan (1989, 1990) kushinda Ligi ya
Klabu Bingwa Ulaya/Kombe la Ulaya misimu miwili mfululizo, na ni mara yao ya 12
kushinda kombe hilo.
Mwaka huu ni
mara ya tatu kwa Real Madrid kufika fainali katika misimu minne.
|
Kipa Gianluigi Buffon.
Juventus ndiyo
klabu pekee ambayo ilikuwa haijashindwa mechi yoyote msimu huu Ligi ya Klabu
Bingwa Ulaya, klabu ya kwanza tangu Atletico Madrid mwaka 2013/2014 kufika
fainali bila kushindwa.
Kushindwa
kwa Juventus ni pigo kubwa kwa nahodha wao, mlinda lango Gianluigi Buffon, 39,
ambaye hajawahi kushinda Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.
Kabla ya
mechi, alikuwa amesema ushindi ungekuwa na maana kubwa sana kwake.
|
No comments:
Post a Comment