Makamu wa
Rais Mhe.Samia Suluhu Hassan akiongea na wananchi (hawapo pichani) katika kilele
cha maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani Jana June 04,2017 Mjini Butiama mkoani Mara.
|
Makamu wa
Rais Mhe.Samia Suluhu akiongea na mjane wa Rais wa Kwanza wa Tanzania Baba wa Taifa
Julius Kambarage, Mama Maria Nyerere (kulia).
|
Viongozi
mbalimbali wakiwa meza kuu.
Makamu wa
Rais Mhe.Samia Suluhu Hassan ameagiza kuchukuliwa kwa hatua kali za kisheria kwa
viwanda na migodi inayofanya shughuli zake za uzalishaji kwa kuharibu mazingira
ikiwamo utitirishaji wa kemikali katika
makazi ya watu.
Amesema kufanya hivyo kunahatarisha usalama wa wananchi
na viumbe hai wengine.
Mama Suluhu
Hassan ametoa agizo hilo Juni 4,2017 kijijini Butiama mkoani Mara wakati akihutubia
wananchi katika kilele cha Siku ya Mazingira Duniani.
Amesema
uharibifu wa mazingira ukiachwa uendee nchini ni hatari kwa usalama wa maisha
na viumbe na hivyo ni muhimu kwa viongozi katika ngazi zote kuchukua hatua
zitakazosaidia kukabiliana na vitendo hivyo.
“Kutozingatia
hifadhi ya mazingira kunaweza kusababisha kuparaganyika kwa mfumo wa
ikolojia na kufanya maisha yetu na ya
vizazi vijavyo kuwa mashakani,” amesema
Aliongeza
kuwa katika kuadhimisha Siku ya Mazingira Duniani viongozi wanapaswa kuchukua
hatua za kuelimisha wananchi na kuwahamasisha ili kila mtu ashiriki katika
juhudi za kuwa na uchumi unaozingatia hifadhi ya mazingira.
|
No comments:
Post a Comment