Rasmi sasa timu
tatu zilizoteremka daraja kutoka Ligi kuu soka Vodacom Tanzania bara msimu huu
2016/2017 zimejulikana nazo ni JKT Ruvu
kutoka Pwani, Toto African ya Mwanza
na African Lyon ya Dar es Salaam.
Toto African wamepoteza kwa kuchapwa mabao 3-1
dhidi ya Mtibwa Sugar wakiwa ugenini
mjini Manungu, Morogoro na Ndanda FC
wakawashindilia zaidi JKT kwa mabao
2-0 ambao tayari walikuwa wameishateremka.
Kwa African Lyon, wao walionekana kama
walikuwa wanaweza kubaki lakini sare yao ya 0-0 ikishindwa kuwaokoa katika mehi
ya mwisho.
Matokeo ya
mechi nyingine Kagera Sugar
imeifunga Azam FC bao 1-0 Uwanja wa
Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam, Stand
United imeilaza 2-1 Ruvu Shooting
Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga na Majimaji
FC imeshinda magoli 2-1 dhidi ya Mbeya City Uwanja Maji Maji Songea.
Hiyo
inamaanisha, JKT Ruvu, Toto Africans na African Lyon ndizo zinaipa mkono wa kwaheri
Ligi Kuu, zikizipisha Mji Njombe, Lipuli ya Iringa na Singida United
zilizopanda kutoka Daraja la Kwanza.
|
Saturday, May 20, 2017
Yanga SC-Mabingwa wa ligi kuu Tanzania bara 2016/2017.
Tags
# MICHEZO
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
MICHEZO
Labels:
MICHEZO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
No comments:
Post a Comment