Bunge la
Tanzani Hapo Jana May 10,2017 limepiga
kura na kuwachagua wabunge wawili wa CHADEMA watakaoungana na wenzao 7 kutoka
CUF na CCM kwa ajili ya kuiwakilisha Tanzania katika Bunge la Afrika Mashariki
(EALA).
Uchaguzi huo
wa wabunge wa CHADEMA ulirudiwa jana baada ya wagombea wa kwanza kukataliwa
bungeni kwa kupigiwa kura ya hapana kwa kile kilichoelezwa kuwa hawakuwa
wamekidhi vigezo.
Katika
uchaguzi wa jana, wabunge wawili waliochaguliwa ni Josephine Sebastian Lemoyan na Pamela Pamela
Maasay.
Katika
kinyang’anyiro hicho wagombea wengine walikuwa nia Ezekiel Wenje, Lawrence
Masha, Salum Mwalimu na Prof. Safari.
Matokeo ni kama ifuatavyo;
1.Abdallah
Safari- kura 35
2-Wenje
-kura 34
3-Lawrence
Masha -kura 44
4-Salim
Mwalimu -kura 54
5- Josephine
Lemoyan -kura 219
6-Pamela
Maasay kura -200
Kufuatia
ushindi wa wagombea hao wawili, wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki sasa
wanafikia 9 ambapo 5 ni wanawake na 4 ni wanaume.
Wabunge 9 wa Tanzania katika Bunge la
Afrika Mashariki ni Pamoja na -
1. Fancy Nkuhi (CCM)
2. Happiness Legiko (CCM)
3. Maryam Ussi Yahya (CCM)
4.Dkt Abdullah Makame (CCM)
5.Dkt Ngwaru Maghembe (CCM)
6. Alhaj Adam Kimbisa (CCM)
7. Habib Mnyaa (CUF)
8. Josephine Sebastian Lemoyan (CHADEMA)
9. Pamela Pamela Maasay (CHADEMA).
|
No comments:
Post a Comment