Video Highlights-Monaco Ikipigwa nyumbani na Juventus 0-2 - Nusu Fainali Champions League 2016/2017. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, May 04, 2017

Video Highlights-Monaco Ikipigwa nyumbani na Juventus 0-2 - Nusu Fainali Champions League 2016/2017.

Gonzalo Higuain akiifungia Juventus bao la kwanza dakika ya 29 kati ya magoli mawili aliyofunga lingine dakika ya 59 katika ushindi wa 2-0 dhidi ya wenyeji, Monaco kwenye Nusu Fainali ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Ulaya 2016/2017 hapo Jana May 3, 2017  Uwanja wa Louis II mjini Monaco, Ufaransa.


Klabu ya Juventus ya Italia imecheza ugenini usiku wa Jumatano hii dhidi ya FC Monaco katika mchezo wa kwanza wa nusu fainali michuano ya Klabu bingwa ulaya na kuchomoza na ushindi wa mabao 2-0.

Mabao ya ushindi ya Juventus yalifungwa na Mchezaji Gonzalo Higuain katika dakika ya 29 kipindi cha kwanza na bao la pili Dakika ya 59 kipindi cha pili, na timu hizo zitarejeana tena mnamo mei 9 mwaka huu.
Baada ya michezo miwili ya nusu fainali ya kuchezwa utafuta mchezo wa fainali utakaopigwa June 03,2017 mjini Cardiff ukizikutanisha timu zilizofuzu hatua ya nusu fainali.

HAPA CHINI TAZAMA VIDEO YA MATUKIO YA MCHEZO KWA KU BOFYA PLAY.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad