Kamishna
Msaidizi Mwandamizi Lazaro Mambosasa, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma
amesema taarifa sahihi ni kwamba hiyo
ndege ni scrapper, ilikuwa ni ndege ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania, ilikuwa
airport na ilishafutwa kwenye ndege za jeshi na ni kopo tu wala haina
engine nzima.
“Muhusika
ambaye aliinunua kwenye mnada jana alikuwa anaikokota kwa kuivuta na tractor kupitia
hiyo hiyo barabara ya airport. Sasa
wakati anaivuta katika kupishana na magari, tairi zikateleza na kuingia kwenye
zile kingo za barabara, baada ya hapo wakaitoa na kuendelea na safari yao. Jana
nikapigiwa kuwa kuna ajali lakini ukweli ni kwamba hakukua na ajali,” Mambosasa
ameimbia Clouds Fm.
No comments:
Post a Comment