Mkuu wa
Jeshi la Polisi wilayani Ngara mkoani Kagera Bw. Abedi Maige amethibitisha
kutokea kwa ajali hiyo na kwamba imesababisha Kifo cha Mtu mmoja ,Majeruhi na
uharibifu wa magari yote mawili
akizungumzia ajali hiyo iliyo tokea katika eneo la Mkafigiri kata ya
mabawe wilayani Ngara mkoani Kagera.
|
Ajali hii ililihusisha gari namba T 738 AEB aina ya Toyota Land Cruiser Mali ya Ngara Oil likiendeshwa na Bw.Said Mikidad ( 37 ) akitokea Kabanga kuelekea Ngara Mjini liligongana na gari lililokuwa likielekea nchini Burundi lenye namba IT 2904 BRD aina ya Toyota RV4 na kusababisha kifo cha dereva wake Ndabashinze Paschal ( 46 ) aliyekuwa akitokea Dar Es Salaam kuelekea nchini Burundi. |
Mashuhuda wakilitizama gari namba T 738 AEB aina ya Toyota Land Cruiser Mali ya Ngara Oil likiendeshwa na Bw.Said Mikidad ( 37 ) akitokea Kabanga kuelekea Ngara Mjini liligongana na gari lililokuwa likielekea nchini Burundi lenye namba IT 2904 BRD aina ya Toyota RV4 na kusababisha kifo cha dereva wake Ndabashinze Paschal ( 46 ) aliyekuwa akitokea Dar Es Salaam kuelekea nchini Burundi. |
Bw. Maige
amesema ajali hiyo imesababisha majeruhi wanne ambao ni Said Mikidad (37)
mwenyeji wa Kabanga,Ngara ( Dereva),Tiberth Selestine ( 27) Afisa Afya Kabanga,
Charles Mdoe ( 41 ) Dereva na Antony John ( 47) Mfanyabiashara mkazi wa Dar Es
Salaam na wote wamelazwa katika Hospitali ya Nyamiaga wakipatiwa matibabu
zaidi.
Chanzo cha
ajali hiyo ni uzembe wa Dereva wa gari la IT
.
|
Mashuhuda wakiliangalia gari lililokuwa likielekea nchini Burundi lenye namba IT 2904 BRD aina ya Toyota RV4 baada ya ajali eneo la tukio na kusababisha kifo cha dereva wake Ndabashinze Paschal ( 46 ) aliyekuwa akitokea Dar Es Salaam kuelekea nchini Burundi. |
No comments:
Post a Comment