Mkuu wa mkoa
wa Arusha, Bw Mrisho Gambo akiwa pamoja na wazazi wa majeruhi wa ajali ya
wanafunzi wa Lucky vicent katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa KIA kabla ya
safari ya kuelekea Marekani kwaajili ya matibabu yaliyotolewa na taasisi ya
Samaritan's Purse, Ajali hiyo iliyotokea wiki iliyopita huko Karatu mkoani Arusha na kupoteza
maisha ya Wanafunzi, walimu na dereva kufikia 35.
|
Ndege ya
Taasisi ya Samaritan's Purse ikiwa katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa
Kilimanjaro mapema leo asubuhi tayari kwa kuruka mpaka Marekani kwaajili ya
kuwapeleka majeruhi wa ajali ya basi la wanafunzi wa Lucky vicent iliyotokea May 6,2017 na kupoteza watu 35 huko Karatu mkoani Arusha,Tanzania.
|
Sehemu ya
ndani ya Ndege ya Samaritan's Purse iliyowabeba majeruhi watatu wa ajali ya
wanafunzi wa shule ya Lucky Vicent ambao leo wamesafirishwa kuelekea nchini
Marekani kwaajili ya matibabu zaidi huku gharama za matibabu hayo yakitolewa na
taasisi ya Sammaritan's Purse.
|
No comments:
Post a Comment