1.Tarehe 4
Aprili, 2017 Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilifanya Uchaguzi wa
kuwachagua Wajumbe Tisa (9) wa Bunge la Afrika Mashariki watakaoiwakilisha
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Bunge hilo.
Katika Uchaguzi huo, Wajumbe
Sita (6) kutoka Chama cha Mapinduzi na Mjumbe mmoja (1) kutoka Chama cha
Wananchi (CUF) walichaguliwa. Wagombea wawili kutoka Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (CHADEMA)walikosa kura za kutosha kuwapatia ushindi.
2.Hivyo,
Bunge linapaswa kufanya uchaguzi kwa mara ya pili ili kuwapata wawakilishi
Wawili (2) kutoka katika Kundi la Vyama vya Upinzani ambapo Chama
Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ndicho chenye hakiya kujaza
nafasihizo.
3.Katika
mazingira hayo na kwa kuzingatia masharti ya Sheria na Kanuni zinazotawala Uchaguzi huo, na kwa
mamlaka niliyonayo kama Msimamizi wa Uchaguzi nilitoa TAARIFA ya
Siku ya Uteuzi na Siku ya Uchaguzi kwenye Gazeti la Serikali Na. 537 la tarehe
21 Aprili,2017.
Taarifa hiyo ilitaja Sikuya Uteuzi(nominationday) wa Wagombea
kuwa ni tarehe 03 Mei, 2017 Saa Kumi Kamili (10:00) Jioni na Siku ya
Uchaguzi(electionday) kuwa nitarehe 10 Mei, 2017.
Hata hivyo,
tarehe 28 Aprili, 2017 Chama cha CHADEMA kiliandikia barua na kuiwasilisha
kwangu siku ya tarehe 2 Mei, 2017 Jioni.
Barua hiyo ilitoa maelezo kwamba muda
waliopewa kuwasilisha majina ya wagombea kupitia kwenye Taarifa hiyo ni finyu
kutokana na kuathiriwa na kuwepo kwa siku za mapumziko ya mwisho wa wiki pamoja
na Sikukuu ya Mei Mosi iliyoanguakia siku ya Jumatatu hivyo, kuwepo kwa ugumu
wa kufanya vikao vyao.
5.Kutokana
na sababu hiyo, Chama hicho kiliomba kuongezewa muda usiopungua wiki mbili ili
kiweze kukamilisha mchakato wa uteuzi wa wagombea, kupata uthibitisho wa uraia
kutoka Idara ya Uhamiaji na uthibitisho wa sifa za kugombea kutoka Tume ya
Taifa ya Uchaguzi kwa mujibu wa Ibara ya 50 (2) ya Mkataba ikisomwa pamoja na
Ibara ya 67 ya Katiba ya Jamhuriya Muungano wa Tanzania,1977.
6.Kutokana
na sababu zilizotolewa, niliongeza muda wa siku 4 kuanzia tarehe 3 hadi tarehe 7
Mei, 2017 ili kukiwezesha Chama
hicho kukamilisha taratibu hizo
za kisheria na
hivyo kukitaka kuwasilisha kwangu majina na nyaraka za
wagombea waliowateua tarehe 8 Mei, 2017 kabla ya Saa Kumi Kamili (10:00) Jioni
ambayo ni Siku ya Uteuzi wa Wagombea(nomination day).
7.Kupitia taarifa
hii, napenda kuujulisha umma
kwamba Chama cha CHADEMA kimewasilisha kwangu majina sita
(6) ya Wagombea wa nafasi mbili za ujumbe wa Bunge la Afrika Mashariki. Kati ya
wagombea hao wanne (4) ni wanaume na
wagombea wawili (2) ni wanawake.
Majina hayo yamewasilishwa kwangu jana
tarehe 8 Mei, 2017 kabla ya mudawaSaa 10 Jionikama nilivyokuwa nimeelekeza.
8.Baada ya
hatua hiyo,nilifanya uchambuzi wa Nyaraka zilizowasilishwa ili kujiridhisha na
uzingatiwaji wa masharti ya uteuzi wa Wagombea kwa mujibu Ibara ya 50 (2) ya
Mkataba, Ibara ya 67 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977,
Kifungu cha 4 (4) cha Sheria ya Uchaguzi wa Wajumbe wa Bunge la Afrika
Mashariki na Kanuni 5 (2), (3) na Kanuni ya 6 ya Nyongeza ya Tatu ya Kanuni za
Kudumu za Bunge,ToleolaJanuari,2016.
Matokeo ya
uzingatiwaji wa masharti
hayo yameainishwa katika Jedwali lifuatalo:
|
No comments:
Post a Comment