Taarifa ya Bunge kuhusu Uteuzi wa Wabunge wa CHADEMA Bunge la Afrika Mashariki. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, May 10, 2017

Taarifa ya Bunge kuhusu Uteuzi wa Wabunge wa CHADEMA Bunge la Afrika Mashariki.

1.Tarehe 4 Aprili, 2017 Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilifanya Uchaguzi wa kuwachagua Wajumbe Tisa (9) wa Bunge la Afrika Mashariki watakaoiwakilisha Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Bunge hilo. 

Katika Uchaguzi huo, Wajumbe Sita (6) kutoka Chama cha Mapinduzi na Mjumbe mmoja (1) kutoka Chama cha Wananchi (CUF) walichaguliwa. Wagombea wawili kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)walikosa kura za kutosha kuwapatia ushindi.

2.Hivyo, Bunge linapaswa kufanya uchaguzi kwa mara ya pili ili kuwapata wawakilishi Wawili (2) kutoka katika Kundi la Vyama vya Upinzani ambapo  Chama  Cha  Demokrasia  na  Maendeleo  (CHADEMA) ndicho chenye hakiya kujaza nafasihizo.

3.Katika mazingira hayo na kwa kuzingatia masharti ya Sheria na Kanuni zinazotawala  Uchaguzi huo, na  kwa  mamlaka  niliyonayo  kama Msimamizi wa Uchaguzi nilitoa TAARIFA ya Siku ya Uteuzi na Siku ya Uchaguzi kwenye Gazeti la Serikali Na. 537 la tarehe 21 Aprili,2017. 

Taarifa hiyo ilitaja Sikuya Uteuzi(nominationday) wa Wagombea kuwa ni tarehe 03 Mei, 2017 Saa Kumi Kamili (10:00) Jioni na Siku ya Uchaguzi(electionday) kuwa nitarehe 10 Mei, 2017.

Hata hivyo, tarehe 28 Aprili, 2017 Chama cha CHADEMA kiliandikia barua na kuiwasilisha kwangu siku ya tarehe 2 Mei, 2017 Jioni. 

Barua hiyo ilitoa maelezo kwamba muda waliopewa kuwasilisha majina ya wagombea kupitia kwenye Taarifa hiyo ni finyu kutokana na kuathiriwa na kuwepo kwa siku za mapumziko ya mwisho wa wiki pamoja na Sikukuu ya Mei Mosi iliyoanguakia siku ya Jumatatu hivyo, kuwepo kwa ugumu wa kufanya vikao vyao.

5.Kutokana na sababu hiyo, Chama hicho kiliomba kuongezewa muda usiopungua wiki mbili ili kiweze kukamilisha mchakato wa uteuzi wa wagombea, kupata uthibitisho wa uraia kutoka Idara ya Uhamiaji na uthibitisho wa sifa za kugombea kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa mujibu wa Ibara ya 50 (2) ya Mkataba ikisomwa pamoja na Ibara ya 67 ya Katiba ya Jamhuriya Muungano wa Tanzania,1977.

6.Kutokana na sababu zilizotolewa, niliongeza muda wa siku 4 kuanzia tarehe 3  hadi tarehe 7  Mei, 2017  ili kukiwezesha  Chama  hicho kukamilisha  taratibu  hizo  za  kisheria  na  hivyo  kukitaka  kuwasilisha kwangu majina na nyaraka za wagombea waliowateua tarehe 8 Mei, 2017 kabla ya Saa Kumi Kamili (10:00) Jioni ambayo ni Siku ya Uteuzi wa Wagombea(nomination day).

7.Kupitia  taarifa  hii, napenda  kuujulisha  umma  kwamba  Chama  cha CHADEMA kimewasilisha kwangu majina sita (6) ya Wagombea wa nafasi mbili za ujumbe wa Bunge la Afrika Mashariki. Kati ya wagombea hao wanne (4) ni wanaume na  wagombea wawili (2) ni wanawake.

 Majina hayo yamewasilishwa kwangu jana tarehe 8 Mei, 2017 kabla ya mudawaSaa 10 Jionikama nilivyokuwa nimeelekeza.

8.Baada ya hatua hiyo,nilifanya uchambuzi wa Nyaraka zilizowasilishwa ili kujiridhisha na uzingatiwaji wa masharti ya uteuzi wa Wagombea kwa mujibu Ibara ya 50 (2) ya Mkataba, Ibara ya 67 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977, Kifungu cha 4 (4) cha Sheria ya Uchaguzi wa Wajumbe wa Bunge la Afrika Mashariki na Kanuni 5 (2), (3) na Kanuni ya 6 ya Nyongeza ya Tatu ya Kanuni za Kudumu za Bunge,ToleolaJanuari,2016.

Matokeo  ya  uzingatiwaji wa  masharti hayo  yameainishwa  katika Jedwali lifuatalo:
TANBIHI:

√-Maana yake sharti husika limetimizwa

10.Uchambuzi huo umebainisha kuwa Wagombea wote wamekidhi vigezo  na  masharti yanayotakiwa kwa  mujibu  wa  Sheria. Hivyo, napenda  kutoa TAARIFA na  KUWATANGAZA wafuatao kuwa Wagombea katika Uchaguzi wa Wajumbe Wawili (2) kupitia Kundi la Vyama  vya  Upinzani kutoka  Chama  cha  CHADEMA  uliopangwa kufanyika tarehe10 Mei,2017:

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad