HABARI KAMILI.
SOURCE: RK, KM (Wito)
ED: AG
DATE: Wednesday, May 24, 2017
KASULU.
Wanafunzi wa
shule za wakimbizi raia wa Burundi kambini Nyarugusu wilayani Kasulu mkoani
Kigoma wameombwa kuzingatia usafi wawapo shuleni ili kujikinga na magonjwa ya
miripuko kambini humo
Wito huo
umetolewa na afisa afya kutoka shirika la Oxfam kambini Nyarugusu Bw Nicolas
Charles akizungumuza wakati wa ziara yake katika shule za wakimbizi raia wa
Burundi kambini humo
Bw Charlas
ameeleza kuwa awali waligawa vyombo vya usafi shuleni lakini wengi wao wamekuwa
hawazingatii taratibu za usafi
Katika ziara
yake afisa afya ametowa msaada wa sabuni za usafi, sabuni za kuogea, mswaki na
dawa ya meno na kuwaomba wanafunzi waliopewa vifaa hivyo kuvitumia kwa malengo
yalio kusudiwa
SOURCE: RK, EM (Muuza madawa ya
kulevya kukamatwa)
ED: AG
DATE: Wednesday, May 24, 2017
KARAGWE
Mtu mmoja
mkazi wa Kayanga wilayani Karagwe mkoani Kagera anashikiliwa na jeshi la polisi
kwa tuhuma za kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya
Adhibitisha
kutokea kwa tukio hilo Mkuu wa jeshi la polisi wilaya ya Karagwe Bw Mika Makanja
amemtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni Peleusi Mishaki mwenye umri wa miaka 39
Bw Makanja
amesema kuwa mtuhumiwa huyo amemkamatwa hivi karibuni akiwa katika maeneo ya
mji mdogo wa Kayanga akiwa na misokoto 78 ya bangi akielekea kuuza
Insert…………Bw Makanja
Cue in…………..Tulimukamata
Cue Out…………madawa
Hata hivyo
amewataka wananchi wilayani Karagwe kuacha tabia ya kulima na kuuza dawa za
kulevya kwa sababu biashara hiyo itawaletea matatizo badala yake walime na
kuuza mazao ambayo ni halali kama vile Maharagwe, Viazi pamoja na Mahindi
SOURCE: RK, WM (Muuza madawa ya
kulevya kukamatwa)
ED: AG
DATE: Wednesday, May 24, 2017
BUKOBA
Wazazi na
walezi mkoani Kagera wametakiwa kuunga mkono utoaji wa dawa za minyoo na
kichocho kwa watoto wao kwa kuhakikisha wanatimiza wajibu wao ili
kufanikisha adhima ya serikali ya
kukabiliana na magonjwa hayo
Kaimu afisa
afya wa mkoa Kagera Bw Gras Ishengoma
ametoa wito huo wakati wa kikao cha kujadili kuhusu tahadhali ya ugonjwa
wa Ebola na utoaji wa dawa hizo kwa
watoto wenye umri wa miaka 5 hadi 14 kikao ambacho kimefanyika katika ukumbi wa mkuu wa mkoa
Amesema kuwa
magonjwa ya minyoo na tumbo bado yako juu ambapo utafiti uliofanyika mwaka 2016
katika halmashauri 4 ambapo shule ya msingi Kasozibakaya iliyopo halmashauri ya
Biharamulo imeongoza kwa asilimia 82 ikifuatiwa na shule ya msingi Ibuga
iliyopo wilayani Ngara kwa asilimia 71
Kwa upande
wake afisa mpango wa taifa wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele
kutoka wizara ya afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto Bw
Osca Kaitaba amesisitiza wazazi na walezi mkoani Kagera kuhakikisha
wanatoa chakula kwa watoto
SOURCE: RK, KK (Ebora)
ED: AG
DATE: Wednesday, May 24, 2017
MWANZA
Mkoa wa
Mwanza Bw John Mongela amesema kuwa mkoa huo ni miongoni mwa mikoa yenye uwezo
mkubwa wa kupata maambukizi ya ugonjwa wa Ebola ikiwa tahadhari haitachukuliwa
mapema
Akizungumza
katika ufunguzi wa kikao Maalumu cha kujadili namna ya kukabiliana na kuchukua
tahadhali ya maambukizi ya ugonjwa huo, Bw Mongela ameema tayari mkoa huo
umechukua tahadhari za kukabiliana nao
Mongela
amesema kuwa uwezekano wa mkoa wa Mwanza kupata maambukizi ya ugonjwa wa
Ebola ni kutokana na kuwa kitovu cha
biashara kwa nchi za ukanda wa maziwa makuu hivyo juhudi za makusudi zinatakiwa
kuchukuliwa ikiwa ni sambamba na utoaji wa elimu kwa wananchi
Insert…………Mongera
Ceuin…………
Ceout…………..
Mganga Mkuu
wa Mkoa wa Mwanza Dr Leonard Suby amesema kuwa Tanzania katika historia yake
haijawahi kuwa na maambukizi ya ugonjwa wa Ebola hivyo ni muhimu kuchukua
tahadhali ya kukabiliana na ugonjwa huo
Kikao hicho
kimewashirikishaa wakuu wa wilaya za jiji la Mwanza, wakurugenzi, viongozi wa
dini,waganga wakuu wa wilaya, mkurugenzi wa utafiti wa magonjwa ya Binadamu na
viongozi wa ulinzi na usalama
SOURCE: RK, JJ (Kufa maji)
ED: AG
DATE: Wednesday, May 24, 2017
GEITA
Mkuu wa Mkoa
wa Geita Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga ameagiza halmashauri ya Wilaya ya
Geita pamoja na wananchi wa kijiji cha Butwa kuweka ushirikiano ili kujenga
shule kwenye kijiji hicho
Hayo
ameyasema wakati akitoa pole kwa wafiwa na jamii ya Kitongoji cha Lulegea Kata
ya Izumacheli kutokana na tukio la wanafunzi watatu wa shule ya msingi Butwa
kufariki wakitokea shuleni kwenda Nyumbani
Kyunga
amesema kuwa ili kuwasaidia wananchi wa Kitongoji cha Lulegea ni vyema wananchi
kujumuika kwa pamoja na kushirikiana ili waweze kujenga shule ambayo
itawasaidia wananfunzi
Bw Tululaza
Kurulaenda ambaye alikuwa amewabeba wanafunzi hao kwenye Mtumbwi ambao umezama
ameelezea kuwa chanzo cha ajali hiyo ni kutokana na watoto kutokutulia wakati
akiendesha Mtumbwi pamoja na hali ya ziwani kutokuwa shwali
Hapo jana
wanafunzi 24 wamezama maji ambapo watatu wamefariki wakitokea shule ya msingi
Butwa iliyopo Kata ya Izumacheli na tayari miili ya watoto hao imezikwa kwenye
kitongoji cha Lulegea
SOURCE: Ikulu, AG (Rpoti)
ED: AG
DATE: Wednesday, May 24, 2017
DAR ES SALAAM
Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Magufuli amevunja bodi ya Wakala wa
Ukaguzi wa Madini Tanzania TMAA na kuagiza iweze kuchunguzwa
Rais
Magufuli amefikia hatua hiyo hii leo Ikulu jijini Dar es Salaam baada ya
kupokea ripoti ya Madini Katika Makontena ya Mchanga kutoka Kamati Maalum
aliyoiunda kuchunguza mchanga ulio katika makontena ya mchanga wa madini
(MAKINIKIA) yaliyopo katika maeneo mbalimbali hapa nchini
Pia amemtaka
waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospiter Muhongo kujitathmini na ikiwezekana
aachie wadhifa huo kutokana na kushindwa kusimami kikamilifu wizara yake na
kupelekea mchanga mwingi wa dhahabu kwenye makontena kuuzwa nje ya nchi
Insert………Magufuli
Cue In
Cue Out
Akiwasilisha
ripoti hiyo mwenyekiti wa kamati ya wataalamu wa jiolojia na uchambuzi wa
kisayansi iliyoundwa Machi 29 mwaka Prof Mruma amesema uchunguzi huo umebaini
uwepo wa madini ya kiasi cha kati ya Shilingi bilioni 829.4 mpaka 1.439
Trillion kwa makontena 277
Insert………Prof
Mruma
Cue In….
Cue Out
XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX
Wasiliana/News Desk, Ngara Kagera.
Chief News Editor
Ms AuleriaGabriel
auleria@radiokwizera.com
Mobile: +255 769722554
|
No comments:
Post a Comment