Kaimu Mkurugenzi wilaya ya Kibondo-Mhe Gabriel Chitupila.
‘’Kila tunapoenda kumuona mwajili wetu ili tupewe stahiki zetu,
tunaambiwa tujisafirishe malipo yote baadae na hapa tuko mitaani na jambo ili
si jema maana kanuni zinasema mfanyakazi anapohamishwa lazima alipwe pesa za
usumbufu, na safari toka kwa mwajili’’ alisema Anthon
Sakata hilo lilihamia katika Baraza la Madiwani kwenye kikao cha robo ya
tatu kilichofanyika jana ambapo Mhe.
Razalo Piter, Diwani kata ya Busunzu alitaka kufahamu hatima ya walimu hao
na wanafunzi mashuleni ambao awapati huduma za masomo mashule kwa muda mrefu
huku kaimu mkurugenzi wa halmashauri hiyo Gabriel Chitupila akidai
atawachukulia hatua walimu wote ambao hawajaripoti vituon kwao kwani walisha
taarifiwa kuwa watalipwa.
|
Mhe.Simon
Kanguye .
Mhe.Simon
Kanguye ,Mwenyekiti wa halmashauri hiyo alimtaka Mkurugenzi kulitazama upya swala la kuwahamisha Walimu
hao kwani linafanyika bila kuwepo bajeti ya kufanya hivyo na nilazima Walimu
walipwe ili waende kwenye vituo vyao vya kazi.
|
Mbunge wa Jimbo la Mhambwe,Mhe. Atashasta Nditiyae.
|
Bw.Ntilo
Nzigu,Mwenyekiti CWT- Kibondo.
Mwenyekiti wa Chama cha Walimu wilayani Kibondo Bw.Ntilio Nzigo
alisema kuwa hali hiyo inawahathili walimu kisaikolojia kwa kulingana na zoezi
la kuhakiki vyeti udhaniwa nao wamo ndani ya kundi la wafanyakazi waliogushi au
watumishi hewa na kulingana na idadi kubwa ya walimu 129 kuwa mitaani ni
kuathili hali ya taaluma mashuleni kwani wanafunzi hawafundishwi kwa siku hi
ambazo walimu wako mitaani.
|
Bi.Anna Bakari- Mwalimu.
|
Bw.Anthon Sakala -Mwalimu.
|
Bw.Lyaki
Majo- Katibu CWT- Kibondo.
Alipotakiwa kueleza hali halisi, Katibu wa chama cha Walimu Kibondo, Bw.
Lyaki Majo alisema walimu wengi na wanashinda mitaani na kila wanapo jaribu
kudai upewa vitisho vya kufukuzwa kazi jambo ambalo ni kuwanyima haki huku mbunge wa Jimbo la Mhambwe, Mhe. Atashasta
Nditiyae akimtaka mkurugenzi kuwarudisha walimu watatu waliiosimamishwa kazi
Haiwezekani serikali inahangaika kutaka kuajili walimu huku wengine
wanafukuzwa bila utaratibu hili si jema bali zifuatwe taratibu za kazi’’
alisema Nditiye
|
No comments:
Post a Comment