Siku moja
baada ya kukamilisha usajili wa kuvidhamini vilabu vya Ligi Kuu Tanzania bara
kwa kuidhamini Singida United baada ya Simba na Yanga, Sport Pesa leo kupitia
Mkurugenzi wao Abbas Tarimba wametangaza kuanzisha mashindano ya Sport Pesa
Super Cup.
1-
Mashindano ya Sport Pesa Super Cup yataanza June 5 2017 na yatakuwa
yakishirikisha timu nane kutoka Kenya na Tanzania zinazodhaminiwa na Sport
Pesa.
2-
Mashindano hayo yatafanyika kwa mfumo wa mtoano na yatafanyika kwa siku 12
pekee, kwa mwaka huu yatafanyika Tanzania na mwakani yatafanyika Kenya.
3- Kwa
Tanzania timu nne zitashiriki ambazo ni Simba, Yanga, Singida United na
Jang’ombe Boys wanaoongoza Ligi ya Zanzibar, wakati timu kutoka nje ya Tanzania
zitakazoshiriki ni FC Leopard, Tusker FC, Nakulu All Stars na Gor Mahia.
4- Michezo
yote itachezwa katika uwanja wa Uhuru Dar es Salaam na mshindi wa michuano hiyo
atapewa zawadi ya Tsh milioni 66 wakati mshindi wa pili atapewa zawadi ya dola
10000 ambazo ni zaidi ya Tsh Milioni 20.
5- Timu zote
nane zitapewa Tsh milioni tano kama ada ya ushiriki na zitakazocheza hatua ya
nusu fainali kila moja itapewa dola 5000 ambazo ni zaidi ya Tsh milioni 10.
6-Marefa
watakaokuwa wanachezesha game hizo sio kutoka Tanzania wala Kenya lengo ni
kuepusha lawama za upande mmoja kuhisi unaonewa, marefa wa Tanzania watakuwepo
pale lakini sio kama waamuzi wa kati.
Sport Pesa Cup
5/6 Singida
united Vs FC leopard
Yanga Vs
Tusker fc
6/5 Simba Vs
Nakuru All Star
Jang`ombe
boys vs Gor mahia
Nusu fainali
tarehe 8
Bingwa wa
mechi kati ya Singida united vs AFC leopard atacheza na bingwa kati ya Yanga na
Tusker
Nusu fainali
ya pili Bingwa wa mechi kati ya Simba na Nakuru all star atacheza na bingwa wa
mechi kati ya Jangombe boyz na Gor mahia
Fainali ni
tarehe 11 Bingwa kupata milioni 60.
Ligi
itadhirikisha timu za Kenya na Tanzania na ligi itashirikisha timu nane na
mshindi atapata dola 30,000 na mshindi wa pili dola 10,000.
|
No comments:
Post a Comment