Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.
John Pombe Magufuli akimpokea Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni Ikulu
jijini Dar es salaam kabla ya kuana Mkutano wa 18 wa wakuu wa Nchi za Jumuiya
ya Afrika Mashariki Mei 20,2017.
|
Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na
kumkaribisha Mhe. Gaston Sindimwo Makamu wa Rais wa Burundi Ikulu jijini Dar es
salaam kabla ya kuanza Mkutano wa 18 wa wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika
Mashariki Mei 20,2017.
Rais John
Magufuli leo May 20, 2017 (Jumamosi) amemkabidhi rasmi uenyekiti wa Jumuiya ya
Afrika Mashariki (EAC), kwa Rais Yoweri Museveni.
Muda mfupi
kabla ya kumkabidhi nafasi hiyo, Rais Magufuli ambaye alikuwa mwenyekiti wa EAC
kwa miaka miwili amewashukuru wanachama wa jumuiya hiyo kwa kumuamini na kumpa
nafasi hiyo miezi michache baada ya kuingia madarakani.
“Mliniamini
mkanichagua licha ya kuwa madarakani kwa muda mfupi,”amesema Rais Magufuli
ambaye aliteuliwa kuwa mwenyekiti wa EAC, mapema mwaka jana 2016.
Rais
Magufuli amesema anaimani na Rais Museveni kuwa atafanya kazi nzuri kutokana na
uzoefu wake.
“Yaliyonishinda
kuyatatua, atayatatua yeye (Rais Museveni),”amesema.
Mara baada
ya kukabidhiwa nafasi hiyo, Rais Museveni ambaye sasa ni mwenyekiti wa EAC
amesema atahakikisha anatumikia nafasi hiyo kwa nguvu na uwezo wake wote.
|
No comments:
Post a Comment