Akikabidhi
ripoti hiyo, Mwenyekiti wa Kamati hiyo Profesa Mruma amemueleza Rais Magufuli
kuwa makontena yaliyofanyiwa utafiti ni 277 ambapo Kamati yake imebaini kuwepo
na ufisadi mkubwa kwenye suala la usafirishaji wa mchanga huo, ambapo kiwango
kikubwa cha dhahabu kimekuwa kikitoroshwa kwenye mchanga huo.
“Kamati
imebaini kuwapo kwa kiwango kikubwa cha dhahabu kwenye makontena ambapo kontena
moja lina wastani wa kilogramu 28 za dhahabu ambapo thamani yake kwenye
makontena zaidi ya 277 yaliyozuiwa bandarini ni kati ya Tsh bilioni 676 hadi
trilioni 1.14.”
“Makinikia
hayo yalikutwa pia na madini ya shaba, silva, chuma na shaba. Kiwango cha Silva
kilikuwa 6kg-7kg kwa kontena moja hivyo kufanya jumla ya 1689kg kwa makontena
277 yaliyozuiwa bandarini.”
“Licha ya
madini mkakati (strategic metals) kuwapo katika makinikia, hazikuwa
zikifahamika na kusababishia serikali hasara.”
“Kamati
imesema mashine ya ukaguzi wa makontena ina matatizo kwani walificha chuma
ndani ya makontena na mashine haikuona. Sababu mashine za ukaguzi bandarini
hazifanyi kazi vizuri, huenda njia hiyo ilitumika pia kutorosha meno ya tembo.”
“Kamati
imependekeza makontena yapimwe vizuri ili kuweza kubaini aina na thamani za
madini yote yaliyomo kwenye mchanga.
Kamati
imependekeza watumishi wa TMAA na Wizara husika wanaohusika na upotevu
wachukuliwe hatua.” alisema Mwenyekiti huyo.
Aidha Mwenyekiti wa Kamati alimkabidhi Rais Magufuli nakala 5 za ripoti
hiyo ambapo amemwambia baadhi ya mambo akiyasoma yatamkera.
|
Wednesday, May 24, 2017
Rais Magufuli- Waziri Muhongo jitahmini kwa kina, ikiwezekana aachie ngazi haraka.
Tags
# HABARI
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
HABARI
Labels:
HABARI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
No comments:
Post a Comment