Sehemu ya
Wafanyakazi waliofika kwenye Sikukuu ya Wafanyakazi Duniani Hapo Jana Mei 01,2017 katika Uwanja wa
Chuo cha Ushirika mjini Moshi mkoani Kilimanjaro.
|
Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitabasamu wakati
Wafanyakazi wa Taasisi mbalimbali za Umma na Binafsi wakiwa katika maandamano
ya Siku ya Wafanyakazi Duniani ambayo nchini yamefanyika Kitaifa katika Chuo
cha Ushirika, Moshi Mkoani Kilimanjaro.
|
Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe Mosi Mei,
2017 amesema Serikali ya Awamu ya tano
imepanga kufanya nyongeza ya kawaida ya
kila mwaka katika mishahara yaani Annual increment, ambayo ilikuwa imesimama
kwa muda mrefu ikiwa ni pamoja na promosheni.
Rais
Magufuli ametoa ahadi hiyo katika Sherehe za siku ya Wafanyakazi duniani
zilizofanyika katika Uwanja wa Chuo cha Ushirika Moshi mkoani Kilimanjaro.
Amesema
uamuzi wa Serikali wa kuanza kutoa promosheni unatokana na kukamilika kwa zoezi
la uhakiki wa Wafanyakazi hewa zaidi ya
wafanyakzi kumi 19,000 walibainika kuwa wafanyakazi hewa.
''Yale mambo
yote yaliyokuwa pending ikiwa ni pamoja na promosheni kwa sababu
tulishindwa, unaweza kupromoti
mfanyakazi hewa hayupo,kwa sababu tungetoa promosheni wakati kuna wafanyakazi
19,000 hewa,maanake tungepromoti na 19,000 na siajabu na watu waliowaandika
mule ndio wangeletwa katika mapendkezo ya promosheni'' amesema Rais Magufuli.
Aidha, Rais
Magufuli amewaonya watumishi ambao wamekuwa wakidanganya umri wa kustaafu ili
waendelee kufanya kazi kwa muda mrefu na kuwa siku zao sasa zimekwisha.
Katika hatua
nyingine Rais Magufuli amepiga marufuku uhamisho wa Wafanyakazi bila kuwalipa
stahili zao kutokana na kuwepo na tabia ya kuwahamisha wafanyakazi bila
kuzingatia taratibu hasa za malipo ya uhamisho.
''Sasa
niwaombe wafanyakazi yeyote akihamishwa hakuna kuhama mpaka umelipwa pesa ya
uhamisho,kuanzia juu mpaka chini,yeyote atakaye kuhamisha mwambie nipe hela
yangu ya uhamisho ninapoenda akishindwa usihame kaa hapohapo ufanye kazi''
Amesema Rais Magufuli.
Amesema
viongozi wengine wamekuwa wakiwahamisha wafanyakazi kwa maslahi binafsi au visasi kutokana na
maendeleo wanayowapata wafanyakzi
Rais Mgufuli
amewahakikishia wafanyakazi kuwa Serikali ya awamu ya Tano itaendelea kuwajali
na kuwa karibu nao katika kutimiza dhana
ya utatu ya ushirikiano kati ya Serikali, Wafanyakazi na Waajiri kwa lengo la
kuleta maendeleo.
Aidha, Rais
Magufuli amewaeleza wafanyakazi mipango mbalimbali anayofanywa na Serikali
katika kuwaletea maendeleo ikiwa ni pamoja na ununuzi wa ndege mpya ,ujenzi wa
Reli ya kisasa, utoaji elimu bila malipo na uboreshaji wa miundombinu katika
kuwaletea maendeleo wananchi.
Sherehe za
Mei Mosi zilizofanyika katika mkoa wa Kilimanjaro pia zimehudhuriwa na Makamu
wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Spika wa
Bunge Mhe. Job Ndugai, Mawaziri, Manaibu Mawaziri, Wabunge na viongozi mbalimbali
wa Chama na Serikali ambapo kauli mbiu inasema,'' Uchumi wa Viwanda uzingatie
kulinda Haki, Maslahi na Heshima ya Mfanyakazi''.
Jaffar Haniu
Naibu
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Moshi,
Kilimanjaro
1 Mei, 2017
|
No comments:
Post a Comment