Mbunge wa
Geita kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Joseph Kasheku Musukuma amezua
mvutano bungeni kufuatia kile alichokisema kuwa wabunge wengi ndani ya Bunge la
Tanzania wamepita kwa waganga wa kienyeji kipindi cha uchaguzi, na kama kuna
ambao hawajapita ni wawili au watatu.
Musukuma
aliyasema hayo alipokuwa akichangia hoja ya Wizara ya Habari kuwa wasanii
wanatumiwa wakati wa uchaguzi lakini baada ya uchaguzi wanatelekezwa bila
msaada wowote.
“Kwa karama
niliyonayo nikiangalia humu ndani (Bungeni) wakati wa uchaguzi ni wawili au
watatu tu hatujapita kwa Waganga.” alisema Joseph Kasheku Musukuma.
Kauli ya
Kasheku ilikuwa wakati akitaka kuonyesha kuwa si wasanii pekee wanaotumika na
kutelekezwa baada ya uchaguzi, bali hata waganga wanatumika tena baada ya
uchaguzi wanasiasa hao hao wanatumia polisi kuwafukuza.
Kufuatia
hali hiyo, Kasheku aliuliza swali, kama serikali haoni kuna umuhimu wa
kuwajengea japo chuo waganga hawa ili waweze kupatiwa elimu japo kidogo.
“Je,
Mheshimiwa Spika, serikali haioni umuhimu wa kujenga chuo cha kuwasaidia
waganga hawa hata kama ni kwa elimu ndogo?
aliuliza Kasheku.
Wakati
mbunge huyo akiuliza swali lake hilo Bungeni, wabunge wengi walisikika wakitaka
anyamaze, huku wengine wakitaka awaombe msamaha kwani wanaamini kauli ya kwenda
kwa waganga si ya kweli.
|
No comments:
Post a Comment