Serikali ya
Tanzania Leo May 3, 2017, imetoa nafasi kwa watumishi wanaodhani kuwa
wameonewa, baada ya kutajwa kwenye orodha ya watumishi wenye vyeti vya kugushi
(feki) waandike barua ya kukata rufaa na kwa katibu mkuu wa wizara ya utumishi
kuanzia kesho ili malalamiko yao yashughulikiwe haraka.
Hatua hiyo
imefikiwa Bungeni mjini Dodoma baada ya Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Katavi,
Rhoda Kunchela kuomba mwongozo wa spika kuhusiana na suala la baadhi ya
watumishi kudai kuwa wameonewa kwenye sakata hilo.
Akitoa
mwongo huo, Kunchela amesema kuwa sakata la vyeti feki limeibua malalamiko
mengi miongozi mwa watumishi waliokumbwa na suala hilo huku wengine wakidaiwa
‘kuchanganyikiwa’ na kupoteza mwelekeo wa maisha.
Akitolea
ufafanuzi suala hilo, Waziri wa Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, Angela
Kairuki amelieleza Bunge kuwa, Serikali imewapa nafasi watumishi wote
wanaodhani kuwa wameonewa kwenye sakata hilo basi waandike barua za rufaa ya
malalamiko yao na waiwasilishe kwa katibu mkuu wa wizara hiyo ili malalamiko
yao yashughulikiwe mapema.
“Kwa wale
ambao wanafahamu kabisa kwamba vyeti vyao ni vya kugushi, wasithubutu kukata
rufaa kwa kuwa ikibainika tena kwamba wamefoji, hatua kali zaidi
zitachukuliwa.” Alisema Kairuki.
BOFYA HAPA
CHINI KUSIKILIZA KAULI YA SERIKALI BUNGENI LEO.
|
No comments:
Post a Comment