Mkurugenzi
mtendaji wa Kampuni ya SportPesa Pavel Slavkov akikabidhiana hati ya
makubaliano ya mkataba na Rais wa Klabu ya Simba Evance Aveva ukiwa ni mkataba
wa udhamini wa kipindi cha miaka mitano wenye thamani ya Bilion 4.9 uliofanyika
leo May 12, 2017 katika ukumbi wa Uwanja wa Taifa.
Kampuni ya
SportPesa imeingia mkataba wa miaka mitano wa kuidhamini klabu ya Simba SC ukiwa
na thamani ya Bilion 4.9 .
Kampuni hiyo
inayojishughulisha na masuala ya michezo ya bahati nasibu nchini Kenya imeweza
kuingia nchini Tanzania na kuja kufanya uwekezaji kwa klabu mbalimbali za mpira
wa miguu.
Utiaji saini
wa makubaliano ya mkataba huo umefanyika jioni hii katika ukumbi wa Uwanja wa
Taifa na kushuhudiwa na wadau mbalimbali wa mpira nchini.
Rais wa
Klabu ya Simba SC, Evance Aveva amesema mkataba huu utaweza kuwasaidia katika
kuendelea kutoa hamasa kwa timu yao kufanya vizuri zaidi.
Kwa upande
wa Mkurugenzi wa SportPesa nchini Abbas Tarimba amesema kuwa wamefurahi sana
kuingia mkataba na Timu ya Simba na mkataba wao utakuwa katika hatua tofauti
kulingana na makubaliano waliyoyaingia.
Amesema kwa
mwaka wa kwanza Klabu ya Simba SC watapata milioni 880 na katika miaka mitatu
inayofuata watapata nyongeza ya asilimia 6
huku mwaka wa mwisho wa mkataba huo klabu hiyo itafaidika kwa kupata
bilioni 1.08.
Mbali na
hilo Tarimba amesema kuwa klabu ya Simba SC itafaidika kwa kupata fedha mbalimbali
kama hamasa iwapo wataweza kupata ubingwa kwa kupewa bonus ya milioni 100 au
kushiriki michuano ya kimataifa.
Kabla ya
utiaji saini wa mkataba huo Simba SC iliweza kutoka na ushindi wa goli 2-1 dhidi
ya Stand United magoli yakifungwa na Juma Luizio yote mawili huku la Stand
United likifungwa na Kasim Selembe.
|
Friday, May 12, 2017
Kampuni ya SportPesa –Rasmi wadhamini Wakuu wa Klabu ya Simba SC.
Tags
# MICHEZO
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
MICHEZO
Labels:
MICHEZO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
No comments:
Post a Comment